Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

April 19, 2018

WATANGAZAJI WA RADIO BEST FM LUDEWA WASHEREKEA PASAKA NA WANAFUNZI WA SHULE MAALUM.

 meneja wa radio best fm akila chakula pamoja na wanafunzi wa shule maalum ya Mundindi




 Bw.Nickson Mahundi akikabidhi misaada mbalimbali kwa walimu ya shule maalumu ya Mundindi
Bw.Nickson Mahundi akikabidhi msaada wa nguo kwa Diwani wa viti maalumu tarafa ya Liganga kwajili ya wanafunzi wa shule maalumu ya Mundindi




Wafanyakazi 90.3 best fm radio Ludewa  kwa kushirikiana na wadau mbalimbali waishio Ludewa mjini wamesherehekea sikukuu ya Pasaka na wanafunzi wa shule maalumu ya Mundindi iliyoko kata ya Mundindi wilayani Ludewa katika mkoa wa Njombe kwa kutoa vitu mbalimbali kwa wanafunzi hao.

Akikabidhi vifaa hivyo zikiwemo Daftari,Dawa za Maswaki,mafuta ya Kupakaa,Sabini na Nguo meneja wa kituo cha radio best fm na Mwenyekiti wa waandishi wa habari wa Mkoa wa Njombe Bw.Nickson Mahundi alisema kuwa kutokana na mahitaji ya wanafunzi wa shule hiyo uongozi wa radio best fm uliona umuhimu wa kuwashirikisha wadau mbalimbali katika kuwasaidia watoto hao.

Bw.Mahundi alisema kuwa shule hiyo pekee Maalumu ya wilaya ya Ludewa ni shule inayotakiwa kuonwa kwa jicho la pekee kutokana na mahitaji halisi ya wanafunzi wanaosoma katika shule hiyo kwani bado jamii haitambui elimu gani inayotolewa katika wanafunzi wanaosoma shuleni hapo.

Alisema kuwa bado jamii haina mwamko wa kuwatembelea wanafunzi hao na kuwajulia hali kutokana na shule hiyo kumilikiwa na Serikali lakini ukweli ni kwamba watoto wanaosoma shule hiyo wanatoka vijiji mbalimbali ndani na nje ya wilaya pia wanatoka katika familia masikini ambazo hazina uwezo hata wakuwatembelea hivyo wadau mbalimbali wanatakiwa kujitolea katika kuwasaidia watoto hao kwa kuwa Serikali inatoa baadhi tu yamahitaji.

“Tumekuja kuwatembelea na kutoa vitu hivi vichache ambavyo ni michango ya wafanyakaji wa wa radio best fm na viongozi wao lakini pia kuna michango ya wadau wa radio yetu wanaoishi Ludewa mjini na vijijini lai yangu ni kwa jamii itambue kuwa hawa wanafunzi ni wetu hivyo tunapaswa kuwasaidia kwani mtoto wa mwenzio ni wako”,alisema Bw.Mahundi.

Naye mwalimu wa shule hiyo Tumaini Mapunda akitoa taarifa ya shule alisema kuwa shule hiyo ina kabiliwa na upungufu mkubwa wa mabweni kwani mabweni yaliyoko hayaendanina idadi ya wanafunzi hali inayo walazimu kuwa na msongamano mkubwa wa wanafunzi ambao nihatari kwa afya zao.

Mwalimu Mapunda alisema kuwa shule hiyo ina wanafunzi wenye ulemavu wa aina mbalimbali kama vile wasioona,wasiosikia,wenye mtindio wa ubongo, wenye ulemavu wa ngozi na wenye ulemavu wa viungo hivyo kuna walimu wenye mafunzo maalumu ambao wana uwezo mkubwa waku wafundisha wanafunzi wao.

Alisema kuwa wazazi wawanafunzi hao wamekuwa na maisha magumu hali inayo sababisha halmashauri  ya wilaya ya ludewa kutumia baeti kubwa katika kuwarudisha makwao shule inapo fungwa na kwenda kuwachukua shule inapo funguliwa aidha aliwashukuru wadau mbalimbali wanao jitolea katika kuwasaidia wanafunzi hao.

Akiushukuru uongozi wa radio Best fm Ludewa kwa kuwatembelea na kutoa misaada kwa wanafunzi hao diwani wa kata ya Mundindi kupitia chama cha mapinduzi (CCM),Mh.Wise Mgina alisema kuwa tokea shule hiyo ianzishwe hakuna waandishi wowote ambao wamewahi kutembelea shuleni hapo.

Mh. Mgina aliupongeza uongozi wa redio Best fm kwa ziara iyo na kuutaka uendelee kuitangaza shule hiyo na changamoto zake katika maeneo mbalimbali ili wadau waweze kujitokeza kutoa misaada na kuiga mfano wa radio Best fm kwani ni wananchi pekee wa kata ya Mundindi ndio wanaowajibika katika ujenzi wa shule hiyo richa ya kuwa kuna wanafunzi wa maeneo mbalimbali.

Mwisho.



No comments: