Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

June 29, 2013

WANANCHI WA KIJIJI CHA NINDI KATA YA LUPINGU WATARAJIA KUNUFAIKA NA HATI ZA ARDHI ZA KIMILA

wajumbe wa kamati ya upimaji wa ardhi katika kijiji cha Nindi kwaajili ya matumizi bora ya ardhi wakiwa picha ya pamoja baada ya kumaliza mafunzo kutoka kwa wataalamu wa ardhi wilaya ya Ludewa
Kikao cha KAMAKA kikiwa kinaendelea katika kijiji cha Nindi kwaajili ya kupata hati za kimila za Ardhi
Afisa ardhi mteule wa wilaya ya Ludewa Bw.Joseph Kamonga akikabidhiwa zawadi maalum kutoka kwa mwenyekiti wa kijiji cha Nindi Bw.Henjewele akiwa na Mkewe


 Vijana wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kupata mafunzo ya kutumia GPS







WANANCHI wa kijiji cha Nindi kata ya Lupingu wilayani Ludewa katika mkoa wa Njombe hivi karibuni wanatarajia kunufaika na hati za kimila katika umiliki wa Ardhi kutokana na wataalamu wa halmashauri ya Ludewa kuanza zoezi hilo katika kijiji hicho.

Akizungumza katika kikao cha kamati ya halmashauri ya kijiji(KAMAKA) kilichofanyika jana kijijini hapo Mwenyekiti wa kijiji cha Nindi Bw.Valentin Henjewele alisema hatua hiyo itaondoa migogoro iliyokithiri kijijini hapo kwa muda mrefu.

Bw.Henjewele alisema viongozi wa kijiji hicho wamekuwa wakipata usumbufu wa kutatua migogoro hivyo hatua iliyofikiwa na Serikali ya kuandaa mpango wa matumizi bora ya Ardhi katika kijiji chake itakuwa ni ukombozi mkubwa hasa kwa raia ambao walikuwa hawajui sheria na mipaka yao.

Alisema upimaji huo wa ardhi na umiliki wa hati za kimila utakuwa ni chachu ya maendeleo kwa vijiji jirani ambavyo bado havijapimwa kwani wataalamu wa ardhi toka wilayani wameweza kufafanua faida za hati hizo ambapo wajumbe wa mkutano huo wamepata shauku ya kumiliki hati hizo.

“Tunaishukuru Serikali kwa suala hili kwani wananchi kupitia hati hizi za kimila wataweza kukopesheka na asasi mbalimbali za kifedha tofauti na miaka ya nyuma tulikuwa tukigombania ardhi bila manufaa yoyote lakini kwa sasa hata migogoro miongoni mwetu ya kuhusiana na mipaka itapungua”,alisema Bw.Henjewele.

Afisa Ardhi Mteule wa wilaya ya Ludewa Bw.Joseph Kamonga mpango wa utoaji wa hati za kimila za umiliki wa ardhi kwa wananchi ni endelevu kwani mpaka sasa tayari vijiji vitatu vimesha pimwa na tayari hati zinaandaliwa.

Bw.Kamonga alisema Serikali imeona umuhimu wa kupima ardhi ya vijiji na kutoa hati kwa wananchi ili kuondoa migogoro isiyo ya lazima kwa wananchi kutokana na thamani ya ardhi inavyoongezeka siku hadi siku.

Mradi huo unasimamiwa na Halmshauri ya wilaya ya Ludewa baada ya kujengewa uwezo na MKURABITA hivyo umeanza kwa vijiji vya mfano ambavyo ambavyo ni Iwela,Aman na Nindi ili kuiwezesha zamii kunufaika na ardhi.

Alisema hati hizo za kimila zitawapa fulsa mbalimbali wananchi kutokana na umuhimu wa hati hizo hivyo mtu yeyote mwenye hati hiyo atakuwa na uwezo wa kukopa fedha bank na kuiwekea dhamana hati hiyo.

Bw.Kamonga alisema licha ya wananchi wa kijiji cha Nindi kunufaika na hati hizo lakini kupitia upimaji wananchi hao wataweza kujifunza sheria za ardhi kutokana na ushiriki wao katika upimaji pia watajua mipaka ya kijiji chao na vijiji vingine kwa ufasaha.

Alisema baadhi ya wananchi wamepata mafunzo ya kutumia vifaa vya upimaji kama gps ambao watashiriki moja kwa moja na wataalamu watakaohusika na zoezi hilo la kupima kuanzia wiki la jumatatu ambapo baada ya kumaliza wananchi wataweza kuandaliwa hati zao na kukabidhiwa.

Aidha aliwataka wananchi hao kuzitunza hati watakazo pata kwani zisipotunzwa inaweza kuibuka migogoro mingine baadae na ushahidi ukakosekana kwa lengo la kutafuta suruhu.

Mwisho.

No comments: