Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

April 22, 2018

KIJIJI CHAKOSA MIUNDOMBINU YA BARABARA TOKEA UHURU MPAKA SASA

 Wananchi wa kijiji cha Nkwimbili pamoja na Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Ludewa Mh.Edward Haule wakichimba barabara ya kuunganisha na makao makuu ya wilaya.

  Wananchi wa kijiji cha Nkwimbili pamoja na Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Ludewa Mh.Edward Haule wakichimba barabara ya kuunganisha na makao makuu ya wilaya.
  Wananchi wa kijiji cha Nkwimbili pamoja na Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Ludewa Mh.Edward Haule wakichimba barabara ya kuunganisha na makao makuu ya wilaya.
 Wananchi wa kijiji cha Nkwimbili pamoja na Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Ludewa Mh.Edward Haule wakichimba barabara ya kuunganisha na makao makuu ya wilaya.
 Mhariri wa Radio Best radio Ludewa Albentino Kayombo akiwa katika kijiji cha Nkwimbili

Mwandishi wa mtandao huu Nickson Mahundi akiwa katika kijiji cha Nkwimbili

Ukosefu wa miundombinu ya barabara katika kijiji cha Nkwimbili kata ya Lupingu wilayani Ludewa mkoa wa Njombe umewafanya wananchi wa kijiji hicho pamoja na viongozi wao kuanza kufikilia mbinu mbadala ili huduma hiyo iweze kuwakomboa baada ya muda mrefu kubeba wagonjwa wao katika machela.

Akiongea na waandishi wa habari jana waliokitembelea kijiji hicho na kushiriki uchimbaji wa barabara kwa jembe la mkono mwenyekiti wa kijiji cha Nkwimbili Bw.Augustino Mlazo alisema kuwa tokea uhuru wa Tanganyika takribani miaka 57 imepita kijiji hicho hakikuwahi kuwa na miundombinu ya barabara.

Bw.Mlazo alisema kuwa wananchi wa kijiji hicho wamekuwa na shauku kubwa ya kuwa na barabra ili kuviwezesha vyombo vya usafiri vikiwemo pikipiki na magari kuingia kijijini hapo hivyo kwa umoja wao wameamua kushirikiana kwa kuanza kuchimba barabara kwa jembe la mkono ili kuweza kuunganishwa na makao makuu ya wilaya ya Ludewa.

Alisema kuwa kijiji hicho chenye changamoto nyingi lakini wananchi kwa pamoja wameona changamoto kubwa ni miundombinu ya barabara  ambayo kukosekana kwa barabara kumewafanya muda mwingi kutembea kwa umbali wa Zaidi ya kilometa 20 kufuata huduma za kijamii.

“tangia nchi hii ipate uhuru mwaka 1961 mpaka leo hatujawahi kuwa na barabara hivyo kutokana na mazingira ambayo tunaishi tumeamua kufanya maendeleo ya kuchimba barabara ili kupata huduma ya usafiri tunamshukuru mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Ludewa kwa kutuunga mkono maana tunashiriki naye katika kazi hii tukitumia jembe la mkono”,alisema Bw.Mlazo.

Aidha Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Ludewa ambaye pia ni Diwani wa kata ya Ibumi Mh.Edward Haule aliwasifu wananchi hao kwa umoja wao bila kulazimishwa na mtu yeyote kwa kujitolea kuchimba barabara hiyo ambayo itawasaidia katika mambo mbalimbali.

Mh.Haule alikili kuwa kijiji hicho tangia Dunia iumbwe hakikuwahi kuwa miundombinu ya barabara hivyo kutokana na umoja wao na kuona barabara ni hitaji la msingi wameanza kuchimba kwa mkono ili kuunganisha na makao makuu ya wilaya ingawa kunachangamoto nyingi ikiwemo ya milima mikali na maporomoko.

Alisema kuwa kutokana na juhudi hizo za wananchi tayari Serikali imewaunga mkono kupitia mradi wa Tasaf kwa kuombea fedha za upanuzi wa barabara hiyo kwani mpaka sasa mashine ya kufanya upanuzi imeshaanza kazi kuanzia Ludewa mjini na imeshafikia katika kitongoji cha Liwili karibu na kijiji hicho cha Nkwimbili.

Mh.Haule aliwataka wadau mbalimbali wa maendeleo hasa wazaliwa wa kijiji hicho waishio maeneo mbalimbani ndani ya nchi na nje kuunga mkono duhudi hizo za wananchi kwani uwepo wa barabara hiyo ni ukombozi mkubwa kwa wananchi wa kijiji cha Nkwimbili kutokana na kadhia wanayoipata ya kubeba wagonjwa kwenye machela pale hali inapokuwa mbaya.

Mwisho.

No comments: