Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

April 19, 2018

MWENYEKITI WA UMOJA WA WAZAZI CCM WILAYA YA LUDEWA AWATAKA WANANCHI KUCHANGAMKIA FULSA.

 viongozi wa umoja wa wazazi wila ya Ludewa wakifanya usafi wa shamba lao








Mwenyekiti wa umoja wa wazazi wa chama cha Mapinduzi wilaya ya Ludewa Bw.John Kiowi amewata wananchi wilayani hapa kuchangamkia fulsa ya kilimo cha Parachichi kutokana na zao hilo kuwa zao la kibiasha na limeanza kuonesha matumaini katika soko la ndani ya nchi na nje.

Hayo alisema jana siku ya jumuhia ya wazazi nchini ambapo kama wilaya ya Ludewa maazimisho hayo yamefanyia kata ya Ludewa mjini katika shamba la jumuiya hiyo lililopo maeneo ya shule ya Sekondari Ludewa ambapo viongozi mbalimbali wa jumuiya hiyo pamona na wananchi walijitokeza kulisafisha shamba lao.

Bw.Kiowi alisema kuwa maadhimisho hayo yalipaswa yafanyike tarehe 6 April mwaka 2018 kutokana na jumuiya hiyo ilianzishwa tarehe 6 April 1955 hivyo kutokana na kuwepo majukumu mengi imelazimu kuazimisha leo tarehe jana kwa kufanya usafi katika shamba la Parachihi.

Alisema kuwa wananchi wa wilaya ya Ludewa bado haijatambua umuhimu wa kilimo za zao hilo tofauti na wilaya nyingine za mkoa wa Njombe kama wilaya ya Wanging’ombe na Njombe Dc ambazo wananchi wake wameanza kunufaika na zao la Parachicchi kwa kujikwamua kutoka katika wimbi la umasikini.

“wilaya ya Ludewa ni kati ya wilaya nchini zenye udongo wenye rutuba nzuri ambao unakubali kilimo za mazao ya aina mbalimbali ukiangalia upende wa milimani ambako kunabaridi kali ni vyema wananchi wake wakajikita katika kilimo cha parachichi lakini kwa upande wa bondeni mwambao wa ziwa Nyasa kilimo cha Korosho kinakubali hivyo nao wanapaswa kuchangamkia fulsa hiyo”,alisema Bw.Kiowi.

Naye katibu wa umoja wa wazazi wilaya ya Ludewa Bi.Veronika Bilia alisema kuwa umoja huo kwa wilaya ya Ludewa umekuwa na miradi mingi zikiwemo shule za Sekondari pamoja na mabwawa ya samaki hivyo ni vyema wazazi wakajua umoja huo ni funzo kwa wazazi walio wengi kutokana na hali halisi ya umuhimu wa mzazi katika familia.

Bi.Veronika alisema kuwa mwananchi yeyote mwenye umri wa kuanzia mika 18 na kuendelea anatakiwa kujiunga na jumuiya ya wazazi bila kubagua jinsi hivyo ofisi ya jumuiya ya wazazi wilaya ya Ludewa inamipango mingi katika miradi endelevu ikiwemo upandaji wa miti ya mbao kwa manufaa ya vizazi vijavyo kama katibu ofisi ipo wazi kwa anayetaka kujiunga na jumuiya hiyo anakaribishwa.

Mwisho.

No comments: