Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

April 27, 2017

UKOSEFU WA MAJI SAFI NA SALAMA SHULE YA SEKONDARI YA CHIEF KIDULILE NI KERO KWA WANAFUNZI.

katikati Mgeni rasmi mwenye skafu ambaye ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Ludewa na Diwani wa kata ya Ibumi Mh.Edward Haule,kulia ni makamu mkuu wa shule Mwalimu Benitho Mahenge na kushoto ni mwenyekiti wa kamati ya shule mwalimu mstaafu Kalo Haule akifuatiwa na diwani wa kata ya Ludewa Mh.Monika Mchilo.


Mh.Edward Haule akifanya harambeeya fedha kwaajili ya kutatua kero ya maji shuleni hapo
 viongozi mbalimbali wakifuatilia maonesho katika sherehe hizo
Mh.Edward Haule akiwa na Makamu mkuu wa shule wakifafanua jambo
 diwani wa kata ya Ludewa Mh.Monika Mchilo akimshukuru mgeni rasmi
hawa nia baadhi ya wahitimu wa kidato cha sita
Wahitimu wa kidato cha sita wakiimba nyimbo za kwaya
Picha ya pamoja ya mgeni rasmi,viongozi wengine pamoja na wahitimu
 Picha ya pamoja ya mgeni rasmi,viongozi wengine pamoja na wahitimu 


Ukosefu wa maji safi na salama katika shule ya sekondari Chief  Kidulile iliyoko katika wilaya ya Ludewa Mkoani Njombe umetajwa kuwa ni changamoto kubwa kwa wanafunzi wa shule hiyo hali inayosababisha wakati mwingine kulazimika kuvunja vipindi ili wanafunzi kwenda kuchota maji mtoni.


Hayo yamesemwa leo katika mahafari ya pili ya kidato cha sita na makamu mkuu wa shule hiyo mwalimu Benitho Mahenge wakati akisoma risala kwa mgeni rasmi ambapo alizitaja changamoto nyingi zinazoikabili shule hiyo ambazo ni ukosefu wa Dahalia,nyumba za walimu,bwalo la chakula na ukosefu wa maji safi na salama.


Mwalimu Mahenge alisema kuwa shule iyo ambayo iko katika makao makuu ya wilaya  imekuwa ni miongoni mwa shule bora wilayani Ludewa ,lakini tatizo la maji safi na salama limekuwa kubwa kwani kuna wakati inawalazimu kuwatoa wanafunzi madarasani ili kutafuta maji ya kuandalia chakula hali ambayo ni kero kubwa kwa wanafunzi hao.


Alisema kuwa tatizo hilo la ukosefu wa maji safi na salama linapelekea baadhi ya wanafunzi kuugua homa za matumbo hivyo alimuomba mgeni rasmi kuliangalia jambo hilo ambalo ni kero kubwa lakini pia bwalo la chakula kwani msimu wa mvua huwa shida kwa wanafunzi hivyo hulazimika kutumia madarasa kama bwalo la chakula.


Akitoa Hotuba yake katika mahafari hayo mgeni rasmi ambaye ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Ludewa Mh.Edward Haule alisema kuwa chule hiyo ni kioo cha wilaya ya Ludewa kutokana na ukweli kwamba ipo makao makuu ya wilaya hivyo ni aibu kuonekana haina maji safi na salama.


Mh.Haule alisema kuwa tayari amewasiliana na Mhandisi wa maji wilaya ya Ludewa na kupewa makisio ya utatuzi wa tatizo la maji chief kidulile ambayo gharama yake haizidi shilingi milioni mbili na Nusu,hivyo alitoa kiasi cha shilingi laki mbili na kuwaomba wageni waliohudhuria mahafari hayo kumuunga mkono ambapo jumla ya shilingi 564000/=zilipatika kama halambee.


Mh.Haule mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Ludewa ambaye pia ni diwani wa kata ya Ibumi aliwaomba wazazi wa wanafunzi wanaosoma katika shule hiyo pamoja na wakazi wa mji wa Ludewa kuichangia shule hiyo ili kumaliza tatizo ambalo ni kero kubwa kwani tayari kiasi kidogo kimeshachangwa katika sherehe hizo za mahafari.


“Naomba wazazi tuungane kutatua kero hii ambayo tunauwezo nayo kwa kuchangishana ili kuwanusuru watoto wetu na homa za matumbo,lakini kwa yale makubwa Diwani wa kata kwa kushirikiana na Mbunge Mh.Deo Ngalawa wanachapa kazi kwa kutafuta wafadhiri mbalimbali ili kuzimaliza kero hizo pia mimi kama mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya na Serikali ya wilaya ya Ludewa tutahakikisha kero hizo zinatatuliwa”,alisema Mh.Haule.


Alisema kuwa tayari kuna mfadhiri amejitokeza kujenga mabweni mawili lakini wananchi wanatakiwa kuandaa mchanga,Tofari na mawe hivyo kinachotakiwa ni kujitoa kwa moyo katika kazi hizo ili kuwafanya wanafunzi wote kuishi bwenini pia aliwataka wanafunzi wanaohitimu kidato cha sita kwenda kujitolea katika shule walizotoka ili kuwasaidia wadogo zao.


Mwisho.



KWA UDHAMINI WA MTANZANIA RESTAURANT, WANAPATIKANA LUDEWA MJINI KATIKA JENGO LA NDICHELIWE.
 KWA CHAKULA SAFI NA BORA UKIFIKA LUDEWA MJINI MTANZANIA RESTAURANT NDIO SURUHISHO PIA KWA CHAKULA CHA MAHARUSI,MISIBA MAHAFARI NA SHEREHE MBALIMBALI
 KWA MAWASILIANO PIGA NO.0758146258 au 0624985168 KWA CHAKULA CHA UHAKIKA.

No comments: