Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

August 22, 2017

MSANII MAARUFU MKOANI NJOMBE ADDY NG’ARI ALIYEIMBA NYIMBO YA MAOMBOLEZO MSIBA WA HAYATI DEO FILIKUNJOMBE ARUDI KIVINGINE.

 Huyu ndiye Addy Ng'ari msanii maarufu wa bongo fleva mkoani Njombe


 Hii ni ngoma mpya anayotarajia kuiachia hivi karibuni itakayotambulika kwa jina la Kidonda changu
 Huyu ndiye Addy Ng'ari msanii maarufu wa bongo fleva mkoani Njombe



Msanii maarufu mkoani Njombe wa muziki wa Bongo Fleva anayejulikana kwa jina la Addy Ng’ari amerudi kivingine,baada ya ukimya wa muda mrefu katika muziki kutokana na kubwana na mambo yakifamilia.

Addy Ng’ari aliwahi kutamba na nyimbo mbalimbali zikiwemo Ua,Nyumba yakupanga,Tanzania nchi yangu,Maisha na ile ya Ni kweli napenda lakini hasa kibao cha Niamini ambacho mpaka leo kibao hicho bado kinatamba katika maeneo mbalimbali nchini na nyimbo hizo zinapatikana katika mtandao wa you tube.

Akiongea na waandishi wa habari Msanii Addy Ng’ari alisema kuwa kumekuwa na uvumi kuwa ameachana na saana baada ya kufiwa na mpendwa wake aliyemdhamini kufanya kazi mbalimbali katika studio kubwa nchini marehemu Deo Filikunjombe lakini yeye bado anafanya sanaa na hivi ameamua kurudi kivingine na kutoa ngoma mbili mfululizo.


Alisema kuwa ni kweli amepata pigo kubwa kuondokewa na Flikunjombe ambaye ndiye alikuwa akimuunganisha na studio mbalimbali na ilimbidi kusimama kwa muda katika sanaa,hivyo amewataka mashabiki wake kutokuwa wanyonge kwani mchango wake kisanaa katika mkoa wa Njombe ni mkubwa kutokana na wasanii wengi wachanga kufuata miondoko yake.

“Ni kweli nimepata pigo kwa kufiwa na mtu aliyekuwa ni msaada kwangu Mh.Filikunjombe na baada ya kupata taarifa za msiba wake ilinibidi kutunga nyimbo ya maombolezo ambayo ndio ilipigwa katika vyombo mbalimbali vya habari na pale msibani na ikanilazimu kusimamisha kazi zangu za sanaa kwa muda,lakini niwaeleze mashabiki wangu nimerudi kivingine wategemee burudani kama kawaida,”alisema Addy Ng’ari.

Addy Ng’ari alisema kuwa tayari ameshatoa kibao kipya ambacho kinatamba mtaani ambacho kinakwenda kwa jina la Umri unasonga na kibao kingine kipo njiani ambacho sio muda mrefu atakiachia kitakachotambulika kwa jina la Kidonda Changu.

Aidha amewataka wasanii wote nchini kudumisha umoja na mshikamani ili kukuza sanaa mkoani hapa kwani kwa kushirikiana na wadau mbalimbali anatarajia kufanya matamasha makubwa katika mikoa mnne ambayo yanalengo la kuibua vipaji vipya  atashirikisha wasanii mbalimbali nchini.

Mwisho.

No comments: