Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

January 28, 2018

PETS KATA YA LUDEWA WAKAGUA MRADI WA MAJI UTAKAO WANUFAISHA WANANCHI WA KIJIJI CHA LUDEWA.

 Meneja wa mamlaka ya maji Ludewa Bw.Mwinuka Gregory akitoa ufafanuzi kwa wajumbe wa Pets
  Meneja wa mamlaka ya maji Ludewa Bw.Mwinuka Gregory akitoa ufafanuzi kwa wajumbe wa Pets


 wajumbe wa pets wakiongea na mkandarasi
 Hili ndilo eneo linalojengwa tank la maji
 Hili ndilo eneo linalojengwa tank la maji
 hiki ndicho chanzo cha maji


  hiki ndicho chanzo cha maji

Wajumbe wa PETS katika kata ya Ludewa Mkoani Njombe wameanza kazi ya kuitembelea na kuikagua miradi ya mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa na serikali ukiwemo mradi mkubwa wa  maji utakao wanufaisha wananchi wa kijiji cha Ludewa mjini.

Akiongea na wanahabari jana katibu wa kamati ya pets Ludewa Bw.Alen Msigwa alisema kuwa PETS ni kamati maalumu inayoundwa na viongozi kutoka Dini na Madhehebu mbalimbali ili kusimamia na kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa eneo husika na kutolea taarifa kwa wananchi katika mikutano ya vijiji.

Bw.Msigwa alisema kuwa kumekuwa na maswali mengi baina ya wananchi wa kijiji cha Ludewa kuhusiana na mradi mkubwa wa Maji ambao ni muhimu kwa wakazi wa Ludewa kutokana na kutokuwa na taarifa sahihi umeanza linin a unatakiwa kukabidhiwa lini kwa wananchi,hivyo kupitia pets wananchi watapata majibu sahihi kutoka kwa wataalamu.

Alisema mradio huo ambao unaghalimu Zaidi ya shilingi milioni mia nne umekuwa ukizungumziwa sana na wananchi kutokana na shauku kubwa ya wananchi hao kujikwamua na tatizo la maji ambalo lilikuwa ni kilio cha wananchi kwa muda mrefu.

“tumetembelea na katika ukaguzi wetu tumeweza kuona maendeleo mazuri katika ujenzi wa mradi huu richa ya kuwa kumekuwa na maneno ya hapa na pale kuwa mkandarasi anacherewesha ujenzi na ndio sababu iliyotufanya sisi kuja kukagua,ukweli ni kwamba mkandarasi yuko vizuri na tunatumaini ataumaliza mradi huu mapema Zaidi”,alisema Bw.Msigwa.

Akitolea taarifa ya mradi huo meneja wa mamlaka ya maji mji wa Ludewa Bw.Gregory Mwinuka alisema kuwa mradi huo wa maji ujulikanao kwa jina la Mdonga unajengwa na kampuni ya Cviliano co.Ltd ya jijini Mwanza ambayo kiuhalisia inaoneka iko vizuri kutokana na maradi huo kujengwa haraka.

Alisema mpaka sasa tayari bomba zimeshatandikwa na zoezi linaloendelea kwa sasa ni ujenzi wa tank kubwa ambalo litasambaza maji katika vitongozi vya Kiyombo,kanisa B,Kanisa A na kitongojo cha Kimbila  kwani wananchi wa vitongoji hivi wamekuwa na uhitaji mkubwa wa huduma ya maji safi na salama baada ya kuikosa kwa muda.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Civiliano Co.Ltd Mhandisi Seleman Waziri akielezea changamoto anazokumbana nazo katika mradi huo alisema kuwa kumekuwa na changamoto katika upatikanaji wa vifaa kutokana na ukweli kwamba wanunuzi wa vifaa ni Iruwasa hivyo vifaa huchelewa kuletwa hali inayomfanya kuchelewesha kazi.

Aidha aliwasifu wananchi wa wilaya ya Ludewa kwa ushirikiano anaoupata kwani maeneo mengine kumekuwa na ugumu wa kazi lakini tofauti na wananchi wa Ludewa ambao mara nyingi wamekuwa wakimfuata na kumshauri pale wanapoona kunadalili ya vikwazo.

Mwisho.


No comments: