Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

August 04, 2015

Nape Asema Wanaohama CCM ni sawa na Mafuta Machafu.......Amtakia Kila la Heri Edward Lowassa


KATIBU wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye amesema wanachama waliokihama chama hicho wamejivua nguo mbele za watu na kwamba wapinzani wanaowachukua wanahangaika na mafuta machafu.

Aidha, amesema aliyekuwa Mbunge wa Segerea na Naibu Waziri wa Kazi na Ajira, Dk Milton Mahanga, alikuwa anatafuta sababu za kuihama CCM na anamtakia kila la heri, yeye na rafiki yake, Edward Lowassa.

Nape aliyasema hayo jana katika mkutano wake na waandishi wa habari katika Ofisi Ndogo ya CCM Lumumba, Dar es Salaam, alipotakiwa kueleza kuhusu kuhama kwa Lowassa na Dk Mahanga ambao wote kwa nyakati tofauti wamekimbilia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Lowassa alijitoa CCM wiki moja iliyopita baada ya kukwama uteuzi wa CCM wa kuwa mgombea wake wa urais na kukimbilia Chadema ambako anatarajiwa kuwa mgombea wake wa urais na kuungwa mkono na Umoja wa Vyama vinne vya Upinzani (Ukawa).

Dk Mahanga naye alijitoa juzi baada ya kukwama katika kura za maoni jimboni Segerea. “Wanahangaika na oil chafu. Hawa ni wale wale kama ilivyokuwa Mrema (Augustino) mwaka 1995, akabebwa kiasi cha Mwalimu Nyerere kusema mwacheni abebwa.

"Hebu jiulizeni wanaona ubaya wanapotoka, lakini mambo yakiwanyookea hawasemi, wakitoka ndio maneno mengi,” alisema Nape. 
 
Alisema kuondoka kwa Lowassa na wengine wachache, si jambo la kwanza kutokea CCM, na pia si la ajabu wala haliwezi kuwa la mwisho huku akimtuhumu Dk Mahanga kuwa alikuwa akitafuta sababu ya kuondoka CCM.

Akizungumzia mchakato wake Mtama, Nape alisema kulifanyika juhudi kubwa za mafisadi kuhakikisha anashindwa, lakini anashukuru ameshinda na kwamba endapo atapitishwa na chama hicho kugombea ubunge, ana hakika atashinda kwani ni mwadilifu na anayezingatia ya chama hicho ikiwamo kupiga vita rushwa.

No comments: