Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

July 06, 2015

MZEE HILALY NKWERA AMGARAGAZA MHANDISI CHAULA UJUMBE WA NEC LUDEWA

 Mzee Hilaly Nkwera Mjumbe wa NEC wilayani Ludewa kwa sasa ambaye alishinda kwa kishindo
 Huyu ndiye Mhandisi Zefania Chaula akiwaaga wajumba baada ya kushindwa katika uchaguzi wa mjumbe wa NEC wilayani Ludewa

Mkuu wa wilaya ya Ludewa Bw.Anatory Choya akimkabidhi cheti Deo Filikunjombe
 Filikunjombe akikabidhiwa cheti
 Huyu ndiye mzee Nkwera Hilaly mjumbe wa NEC kwa sasa wilayani Ludewa


  wajumbe wa mkutano mkuu Ludewa wakifuatilia mkutano

Mzee Hilaly Nkwera ambaye ni mwanasiasa mkongwe wilayani Ludewa katika Mkoa Njombe amemgaragaza vibaya Mhandisi Zefania Chaula katika uchaguzi wa kugombea nafasi ya halmashauri kuu ya Chama cha mapinduzi (CCM) NEC kwa kura 43 kwa 11ambazo alizipata mpinzani wake.


Uchaguzi huo wa mjumbe wa NEC wilayani Ludewa umefanyika baada ya aliyekuwa mjumbe wa Nec wilayani hapa Elizabeth Haule kufariki Dunia na wilaya ya Ludewa kukosa mwakirishi katika Halmashauri kuu ya CCM Taifa.


Akiwashukuru wajumbe kwa kuibuga mshindi katika uchaguzi huo Mzee Nkwera alisema kuwa amefurahishwa na kitendo cha wanaccm wilayani Ludewa kuendelea kumwamini katika utendaji ndani ya Chama cha mapinduzi hivyo atatumia uwezo na akili yake yote katika kulitumikia taifa na wanaludewa.


Aidha Mhandisi Chaula alikiri kushindwa vibaya katika uchaguzi huo na kuahidi kuwa hatagombea nafasi hiyo tena katika maisha yake kwani ni zaidi ya mara moja amekuwa akigombea nafasi hiyo na kugaragazwa vibaya.


“Nasema haya kutoka moyoni mimi ni mwanachama hai wa chama cha mapinduzi na nakipenda chama change hivyo naahidi sitagombea tena katika maisha yangu nafasi hii ya unec kutokana na ukweli kuwa nahisi siasa inanikataa maana kila nikigombea nashindwa hivyo ngoja nifanye kazi nyingine pia namtakia kila laheri mzee Nkwera katika utendaji wake ndani ya chama”,alisema Mhandisi Chaula.


Katika mkutano huo wa halmashauri kuu ya wilaya ya Ludewa ya Chama cha mapinduzi Mkuu wa wilaya ya Ludewa Bw.Anatory Choya aliweza kumtunuku cheti cha heshima mbunge wa jimbo la Ludewa Mh.Deo Filikunjombe kwa kushiriki kimamirifu katika mbio za mwenge wa Uhuru ndani ya mkoa wa Njombe.


Akitoa cheti hicho Bw.Choya alisema kuwa kutokana na ushiriki alioufanya mh.Filikunjombe katika mbio cha mwenge wa Uhuru mkuu wa mkoa wa Njombe na ofisi yake wameona wampatie cheti cha heshima Filikunjombe kwani ni mbunge pekee aliyeshiriki katika mbio hizo za Mwenge katika mkoa wa Njombe.


Mbunge huyo wa jimbo la Ludewa Mh.Filikunjombe amekuwa kinara wa kushiriki katika kazi za maendeleo ndani ya mkoa wa Njombe na katika jimbo lake hivyo alishiriki kikamirifu katika mbio za Mwenge wa uhuru na hali ambayo iliwafanya wananchi kujitokeza kwa wingi katika kumuunga mkono Filikunjombe kushiriki mbio za mwenge wa uhuru.


Mwisho.

No comments: