Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

July 03, 2015

MWENGE WA UHURU WAZINDUA MIRADI YENYE THAMANI YA ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 1.3 WILAYANI LUDEWA.


 Mkuu wa wilaya ya Ludewa Bw.Anatory Choya akikabidhiwa Mwenge wa Uhuru na Mkuu wa wilaya ya Njombe Bi.Sarah Dumba



Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru mwaka 2015 Bw.Juma Khatibu Chum akiongea na wananchi
 Mbunge wa jimbo la Ludewa Mh.Deo Filikunjombe akiongea na wananchi
Filikunjombe akiupokea mwenge wa Uhuru



 Shamba la miti katika kijiji cha Lupanga ambalo lilizinduliwa na mbio za Mwenge wa Uhuru
Mkuu wa wilaya ya Njombe Bi.Sarah Dumba akimkabidhi mkuu wa wilaya ya Ludewa Bw.Anatory Choya


Vijana wa kundi la sanaa la Ludewa mjini IVA YOUTH GROUP wakipagawisha katika mapokezi ya Mwenge wa Uhuru.
 Filikunjombe akisalmiana na kiongozi wa mbio za mwenge wa Uhuru Bw.Juma Khatibu Chum




Mbio za mwenge wa uhuru zinazoendelea kuzunguka nchi nzima zimeweza kuzindua miradi ya maendeleo wilayani Ludewa katika mkoa wa Njombe yenye thamani zaidi ya shilingi billion 1.3,miradi hiyo ikiwa ni pamoja na kuzindua zahanati,madarasa na kuweka mawe ya msingi katika shamba la miti na nyumba ya kulala wageni.


Mbio hizo za Mwenge ambazo zilikimbizwa katika tarafa ya Mlangali uongozi wa wilaya ya Ludewa ulizipokea kutoka wilaya ya Njombe kijiji cha Lusitu na ziliweza kupokelewa kwa shangwe ndelemo na umati wa wakazi wa tarafa hiyo ambapo mkesha wa mwenye wa Uhuru ulifanyika katika makao makuu ya kata ya Mlangali na baadae wilaya ya Ludewa uliwakabidhi wilaya ya Wanging’ombe.


Akiupokea mwenge wa Uhuru mkuu wa wilaya ya Ludewa Bw.Anatory Choya kutoka kwa mkuu wa wilaya ya Njombe Bi.Salah Dumba alisema kuwa Mwenge wa uhuru ni nuru ya matumaini kwa watanzania hivyo kila mtanzania anapaswa kuuheshimu na kuuenzi kutokana na kazi kubwa ya mwenge wa uhuru katika Taifa letu.


Bw.Choya alisema kuwa wananchi wa wilaya ya Ludewa wanaimani kubwa na Serikali yao katika kuwaletea maendeleo na ndio maana walijitokeza kwa wingi katika kuulaki Mwenge wa Uhuru na umeweza kuzindua miradi mikubwa ambayo imebiniwa na wananchi kwa kushilikiana na halmashauri ya wilaya ya Ludewa pamoja na Mbunge wa jimbo la Ludewa Mh.Deo Filikunjombe.


“Mwenge wa Uhuru umeweza kuzindua miradi mikubwa ya maendeleo yanye thamani ya shilingi Bilioni 1 na milioni 350 ambayo imetekelezwa na nguvu za wananchi kwa kushirikiana na Halmashauri ya wilaya ya Ludewa pamoja na Mbunge wa jimbo la Ludewa hivyo wananchi wanafuraha kubwa kuona miradi yao inazinduliwa na Mwenge”,alisema Bw.Choya.


Akiongea na wananchi wa kijiji cha Mangalanyene ambako Mwenge wa uhuru ulizindua Zahanati Mbunge wa jimbo la Ludewa Mh.Deo Filikunjombe alisema kuwaujenzi wa jengo hilo la Zahanati umegharimu kiasi cha shilingi milioni 40 ikiwa milioni 20 ni mchango wa nguvu zake na shilingi milioni 20 ni mchango wa nguvu za wananchi na Halmashauri.


Mh.Filikunjombe alisema kuwa wananchi wa wilaya ya Ludewa ni wachapakazi hivyo amekuwa wakifanya kazi kubwa za kimaendeleo na wamekuwa na furaha kubwa kuona miradi waliyoifanya kwa nguvu zao inazinduliwa na Mbio za mwenge wa uhuru.


Akifungua miradi hiyo kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa mwaka 2015 Bw.Juma Khatibu Chum alisema kuwa ujembe wa Mwenge wa Uhuru mwaka 2015 ni Kutumia haki yako ya kidemokrasia,jiandikishe na kupiga kura katika uchaguzi wa mwaka 2015 pia vijana wa leo na ukimwi wazazi tuwajibike,wekeza katika maisha ya baadae  tokomeza maralia.


 Bw.Chum alisema kuwa pia ujumbe wa Mwenge wa uhuru unasema “uteja wa dawa za kulevya unazuilika na kutibika chukua hatua,kata mnyororo wa Rushwa chagua kiongozi mzalendo”,hivyo wananchi wanatakiwa kuutumia ujumbe wa Mwenge wa Uhuru katika uchaguzi uchaguzi mkuu wa mwaka huu.


Mwisho.

No comments: