Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

June 20, 2015

MJUMBE WA HALMASHAURI KUU YA MKOA NA MCHUMI WA KATA YA LUGARAWA AHIMIZA MAENDELEO BILA KUJALI ITIKADI ZA VYAMA VYA SIASA.

hizi ni baadhi ya Nondo alizozitoa Bw.Mwapinga
Bw.Mwapinga mwenye fulana ya rangi ya Kijani akimkabidhi mipira mwenyekiti wa kijiji cha Shaurimoyo Bw.Mwinuka

Bw.Mwapinga akimkabidhi jezi mwenyekiti wa kijiji cha Shaurimoyo Bw.Adriano Mwinuka

Bw.Mwapinga akimkabidhi saruji mwenyekiti wa kijiji cha Shaurimoyo Bw.Mwinuka

 Bw.Mwapinga akipongezwa na mabalozi wa Shaurimoyo
hawa ndio mabalozi wa kijiji cha Shaurimoyo kata ya Lugarawa wilayani Ludewa


  hili ndilo jengo la shule ya msingi shaurimoyo ambalo wafadhiri mbalimbali wanalichangia ukarabati wake

Mjumbe wa Halmashauri kuu ya mkoa wa Njombe na mchumi wa kata ya Lugarawa kupitia chama cha Mapinduzi Bw.Damian Mwapinga amewataka viongozi wa chama cha mapinduzi katika ngazi ya vitongoji,vijiji hadi kata kuhimiza uletaji maendeleo kwa wananchi bila kujari itikadi ya vyama vya siasa.


Bw.Mwapinga aliyasema hayo jana katika kijiji cha Shaurimoyo kata ya Lugarawa wilayani Ludewa wakati akiongea na mabalozi wa nyumba kumi ambapo aliweza kutoa vifaa vya ujenzi ambavyo ni saruji mifuko kumi na nondo rolu nne vyote vikiwa na thamani ya shilingi 340000% pia alitoa vitaa vya michezo ambavyo ni jezi seti moja na mpira mmoja kwa timu ya mpira wa miguu Shaurimoyo.


Alisema kuwa wananchi wanahitaji maendeleo na sio malumbano ya kisiasa hivyo yeye kama kada wa chama cha mapinduzi ameona umuhimu wa kuleta maendeleo kwa wananchi ni pamoja na kupunguza umaskini hivyo aliuomba uongozi wa kijiji kutumia nondo na saruji hiyo katika ukarabati wa shule ya msingi shaurimoyo.


Bw.Mwapinga aliwataka viongozi wa vitongoji, mashina na vijiji kuungana na wananchi ili kufanikisha suala zima la maisha bora kwa wananchi kwani kumekuwa na shida kubwa inayosdababishwa na baadhi ya vyama vya siasa ambavyo vimekuwa vikiwashauri wananchi kutofanya kazi za kimaendeleo kwa kusema maendeleo yataletwa na Serikali.


"nawaomba viongozi wenzangu kushiriki katika uletaji wa maendeleo kwa wananchi ambao wanakiu ya maendeleo na sio siasa ambazo zianarudisha nyuma maendeleo na hivi vifa ninavyovitoa nawaomba kama viongozi wenzangu kuvisimamia vifaa hivi ili vitumike kwa malengo yaliyokusudiwa na wananchi waone mazuri ya Serikali yao inayoongozwa na ccm",alisema Bw.Mwapinga.


Akipokea vifaa hivyo mwenyekiti wa kijiji cha Shaurimoyo Bw.Adriano Mwinuka amesema kuwa jamii ya Shaurimoyo imevipokea vifaa hivyo kwa mikono miwili kutokana na wananchi hao kuchangishana fedha za kununulia saruji na nondo kwa muda mrefu bila mafanikio hivyo gharama za manunuzi zitapungua kutokana na mjumbe huyo kuchangia sehemu ya vifaa hivyo.


Bw.Mwinuka amesema kuwa  vifaa hivyo vitatumika kwa ukarabati wa majengo ya madarasa ambayo yalijengwa kwa muda mrefu na mbao za majengo hayo zimeliwa na mchwa ambazo zinaweza kuleta madhara kwa wanafunzi hasa msimu wa mvua unapowadia.


Aliwataka wadau mbalimbali kuendelea kuchangia ujenzi wa shule hiyo ambayo imekuwa ikihitaji ukarabati kwa muda mrefu bila mafanikio kutokana na michango ya wananchi kutotoshereza katika ununuzi wa vifaa vinavyohitajika hivyo kama watatokea wadau kama Bw.Mwapinga itakuwa ni vizuri na italeta tija kwa wananchi.


mwisho.


No comments: