Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

January 29, 2015

WANANCHI LUDEWA WASHAURIWA KUACHA UNYANYAPAA KWA WAGONJWA WA UKIMWI




Wananchi wilayani Ludewa katika mkoa wa Njombe wameshauriwa kutoendekeza tabia za unyanyapaa kwa wagonjwa wanaoishi na virusi vya ukimwi kwa kuwatungia majina mbalimbali kwani hakuna binadamu anayetambua aina ya kifo atakachokufa nacho.


Akizungumza katika mkutano wa watendaji wa Serikali na wajumbe wa uongozi wa kijiji cha Ludende wilayani hapa mganga mkuu wa Zahanati ya Ludende Dkt. Zahao Mtafya amesema kuwa katika kata ya Ludende kuna zaidi ya wagonjwa wa Ukimwi wanaochukua dawa za kufubaza makali ya virusi vya ukimwi lakini kutokana na kuonekana waziwazi wakipanga foleni kuchukua dawa hizo jamii inawanyanyapaa kwa kuwaita majina mbalimbali wasiyo yapenda.


Dkt. Mtafya amesema kuwa awali wagonjwa hao walikuwa katika hali mbaya na wengine wamepoteza maisha kutokana na kunyanyapaliwa pia kata hiyo kutokuwa na vipimo vya kupima CD4 lakini kwa sasa hali imeanza kutengamaa kwa baadhi ya wagonjwa kwani Serikali kupitia mradi wa Tunajali wameweza kununua mashine hiyo na huduma inaendelea pia wanaoishi na wagonjwa hao wanapata elimu ya kupunguza unyanyapaa


Mmoja wa wananchi wa kijiji cha Ludende Bw.Vasco Mgimba alikili kuwepo kwa tabia za unyanyapaa lakini aliwataka wanaotumia dawa za kufubaza virusi vya ukimwi mara baada afya zao kutengamaa kuacha tabia ya kusambaza virusi hivyo kwa makusudi kwa lengo la kulipiza visasi kwa waliowanyanyapaa.


Mwisho.








No comments: