Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

December 22, 2014

MPANGO WA UJENZI WA MAABARA KATIKA SHULE ZA SEKONDARI WILAYANI LUDEWA WAFANIKIWA KWA ASILIMIA TISINI.




Imeelezwa kuwa mpango wa uzenzi wa maabala katika shule za Sekondari wilayani Ludewa katika mkoa wa Njombe umekamilika kwa asilimia tisini kutokana na ukweli kwamba idadi kubwa ya shule wilayani hapa zimekuwa na majengo ya kutosha hivyo kuwa vyumba vya ziada ambavyo vimefanywa kuwa maabala hizo


Akitoa taarifa ya mpango huo wa ujenzi wa maabara kwa waandishi wa habari jana ofisini kwake  Ofisa elimu wa shule za Sekondari wilaya ya Ludewa Bw.Matenus Ndumbalo alisema mpango huo umefanikiwa kwa asilimia tisini kwani katika shule za Sekondari wilayani Ludewa ni shule mbili pekee ndizo zilizokosa vymba vya ziada.


Bw.Ndumbalo alizitaja shule ambazo zimekosa vyumba vya ziada na kulazimika kuaandaa bajeti ya ujenzi wa majengo mengine ya maabara ni pamoja na shule ya sekondari ya Ketewaka na ile ya Makonde lakini nyingine zimekamilisha ukarabati wa vyumba na tayari baadhi ya shule vifaa hivyo vya maabara vimeshawasili tayari kwa kuanza kufundishia wanafunzi.


Alisema kuwepo kwa vyumba vya ziada kumesababishwa na kupungua kwa idadi ya wanafunzi katika shule hizo chanzo kikiwa ni mitihani ya kidato cha pili kwani wanaoshindwa kufaulu hugoma kurudia kidato cha pili na kujikita katika shughuri za kilimo hivyo madarasa hubaki wazi.


“Tumekuwa na vyumba vya madarasa visivyo na kazi hali ambayo imeturahisishia kuvitenga vyumba hivyo kwaajili ya maabara lakini bado tunachangamoto kubwa kwani kumekuwa na idadi ndogo ya wanafunzi wanaopanda kidato cha tatu kutokana na kutofaulu mtihani wa kidato pili na kufanya shule kuwa na idadi ndogo ya wanafunzi”,alisema Ndumbalo.


Akitoa mfano wa upungufu wa wanafunzi  Bw.Ndumbalo aliitaja shule ya Sekondari Ketewaka ambayo iko katika kijiji cha kimelembe kata ya Nkomang’ombe kuwa ni moja ya shule zilizoathirika na mtihani wa kidato cha pili hivyo kukasababisha wanafunzi wa kidato cha nne kufanya mtihani katika shule nyingine.


Licha ya kukamilisha kazi ya ujenzi wa Maabara kwa asilimia tisini pia alizitaja changamoto zinazomkabili katika idara yake wilayani hapa ni pamoja na ukosefu wa Walimu wa masomo ya Sayansi  na walimu wa kike katika baadhi ya shule ambazo zinadahalia.


Alisema wilaya ya Ludewa ni moja ya wilaya zenye wanafunzi wenye vipaji kutokana na kutumia vyakula vya asili na Samaki wa ziwa nyasa lakini wanashindwa kufanya vizuri katika masomo ya sayansi kutokana na ukosefu wa walimu wa masomo hayo hali ambayo imekuwa ni changamoto ya kila mwaka.


Bw.Ndumbalo alisema licha ya kuwa katika baadhi ya shule ya Sekondari ujenzi wa maabara na vifaa vyake umekamilika lakini hakuna walimu wa masomo ya Sayansi jambo ambalo bado linawaumiza vichwa viongozi wa wilaya ya Ludewa pale wanapokutana katika vikao ili kujadili hali ya Elimu katika wilaya.


Changamoto nyingine ambayo imekuwa ikiitesa idara ya elimi ni ile ya ukosefu wa walimu wa kike katika baadhi ya shule za sekondari na mfano wa moja ya shule hizo ni shule ya Sekondari Makonde ambayo ina dahalia lakini haina mwalimu wa kike ambaye angeweza kuwa jirani na wanafunzi wa kike hali ambayo inasababisha walimu wa kiume kusikiliza matatizo ya wanafunzi wa kike.


Bw.Ndumbalo alisema suala kuokuwa na walimu wa kike katika shule za Sekondari limesababishwa na baadhi ya shule kutokuwa na Nyumba za walimu  hivyo aliwataka wananchi kujitolea katika ujenzi wa shule hizo ili walimu waweze kupata mahali pa kuishi.


Mwisho.

No comments: