Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

December 23, 2014

MJUMBEA WA NEC LUDEWA AWATAKA VIONGOZI WALIOCHAGULIWA KUVUNJA MAKUNDI.





Mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Taifa(NEC) wilayani Ludewa katika mkoa wa Njombe Bi.Elizabeth Haule amewataka viongozi waliochaguliwa na wasiochaguliwa katika uchaguzi wa Serikali za mitaa uliofanyika hivi karibuni kuvunja makundi na kuendelea na majukumu ya kulijenga taifa katika kipindi hiki cha sherehe za Chrismas na Mwaka mpya.


Bi.Elizabeth ameyasema hayo leo katika ofisi za CCM wilaya ya Ludewa wakati akiongea na waandishi wa habari waliotaka kujua hali ya wagombe wa chama cha mapinduzi ambao hawakuweza kuchaguliwa na wananchi na wengine walioshindwa katika kura za maoni ndani ya chama.


Alisema hali halisi ya wagombea walioshindwa uchaguzi katika kura za maoni na zile za wananchi iko vizuri kwani asiyekubali kushindwa si mshindani hivyo haina sababu ya kuendelea na makundi badala yake kukaa pamoja na kutekeleza majukumu ya chama na Taifa kwa ujumla ili kuleta maendeleo kwa wananchi.


Bi.Elizabeth alisema wilaya ya Ludewa inajumla ya vijiji 77 katika vijiji hivyo chama cha Mapinduzi kimeweza kushinda nafasi ya uenyekiti wa vijiji 67 na vijiji 10 vimeweza kuchukuliwa na vyama vya upinzani hali inayoonesha kuwa chama cha Mapinduzi kinakubalika na wananchi wa wilaya ya Ludewa na Taifa kwa ujumla.


“Tumeshinda kwa kishindo katika uchaguzi wa Serikali za mitaa ila ninachowaomba wanaccm wenzangu kuvunja makundi ya uchaguzi uliopita na kukijenga chama kwaajili ya kujiandaa uchaguzi mkuu mwaka 2015 pia nawaomba vijana wenzangu kuniunga mkono mwakani kwa kuchukua fomu za kugombea nafasi za Udiwani”,Alisema Bi.Elizabeth.


Alisema licha ya uchaguzi kumalizika bado kunabaadhi ya watu wanaendelea kukumbatia itikadi za vyama hali ambayo si sahihi kwani katika msimu huu wa sikukuu ni vyema kuweka itikadi za kisiasa pembeni na kusheherekea kwa pamoja kama ilivyozoeleka katika tamaduni za kitanzania.


Bi.Elizabeth alisema kumekuwa na wanasiasa wasio wa vumilivu hivyo wanaposhindwa kuchaguliwa ama kukosa lidhaa kwa wananchi ya kushika uongozi huanza kuhama vyama na kuvichafua vyama vingine mtu wa namna hiyo anakuwa hajakomaa kisiasa kinachotakiwa ni kuwa watulivu na kujaribu kwa kipindi kingine.


Mwisho.

No comments: