Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

August 22, 2014

SIMBA WAWILI KUTOKA WILAYANI NYASA WAUA NG'OMBE WATATU WILAYANI LUDEWA.



Simba wawili wanaosadikika kutokea mkoa jirani wa Ruvuma  wameningia katika kijiji cha Ngelenge kata ya Ruhuhu wilayani Ludewa katika mkoa wa Njombe na kusababisha hasara kwa wafugaji baada ya kuwauwa Ng'ombe watatu na kutoweka wakielekea kijiji cha Lituhi wilayani Nyasa.

Akizungumza kwa njia ya simu ya kiganjani na mwandishi wa mtandao huu Ofisa mtendaji wa kata ya Ruhuhu Bw.Asheri Lufingo alisema simba hao ambao walitokea wilayani Nyasa katika mkoa wa Ruvuma walivuka mto Ruhuhu usiku wa Agost 21 mwaka huu na kuingia kijiji cha Ngelenge wilayani Ludewa ambapo waliwaua Ng'ombe watatu na kuwala.

Bw.Lufingo alisema kabla ya kuvuka wilayani Ludewa waliweza kupita maeneo ya Liuli mpaka kufikia Lituhi ambako walikula Ngo'ombe watatu na Nguruwe mmoja ndipo wakafika Ngelenge na kufanya uharibifu mwingine tena.

Anasema tayari taarifa zimesapelekwa maeneo husika na jeshi la polisi kwa kushirikiana na ofisi ya maliasili wanafanya utaratibu wa kuwatafuata ili waweze kuwateketeza kwani wamekiwa hatari kiasi kwamba wananchi wa maeneo husika wanashindwa kufanya shughuri za kimaendeleo wakihofia kudhurika na simba hao.

endelea kufuatilia mtandao huu kwa taarifa zaidi.

No comments: