Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

August 19, 2014

MBUNGE WA ZAMANI LUDEWA STANLEY KOLIMBA AWASHANGAZA WANANCHI

Bw.Stanley Kolimba aliyekuwa mbunge wa jimbo la Ludewa na baadae kuwa mkuu wa wilaya ya Tarime ambaye kwa sasa ni mwenyekiti wa CCM wilaya ya Ludewa akiongea na wananchi wa kijiji cha Manga kata ya Madilu
Filikunjombe na Lugola wakimkabidhi spika paroko wa parokia ya Manga


vijana wa kijiji cha Ilawa kata ya Madilu wakiwa wamevaa mifuko ya nailoni yenye ujumbe wa Deo Filikunjombe Jembe letu
Umati wa watu wa kijiji cha Manga kata ya Madilu uliofika kumpokea  Filikunjombe
Filikunjombe akipokea zawadi ya matunda kwa wananchi wa Manga
Filikunjombe akikabidhiwa zawadi ya Viazi
Filikunjombe akikabidhiwa zawadi ya Mbuzi kutoka kwa wananchi wa Manga
Filikunjombe akimkabidhi diwani Libato wa kata ya Madilu Saruji mifuko 200 na bati 400 kwaajili ya ujenzi washule
Filikunjombe akiongea na wananchi wa Manga
Filikunjombe akiwa na madiwani wa viti maalumu
Filikunjombe wakitoa zawadi ya viatu kwa kwaya ya watoto wa kijiji cha Ilawa walioimba vizuri



Aliyekuwa mbunge wa Ludewa, Stanley Kolimba amewashangaza wananchi wa kijiji cha Manga, Kata ya Madilu wilayani Ludewa baada ya kuwaeleza kuwa anaungama dhambi zake mbele yao.

“Leo na ungama dhambi zangu mbele ya baba Paroko hapa mbele yenu, mimi hili kanisa nalifahamu siku nyingi, na limejengwa tangu mwaka 1968 na nilikuwa napita kwa nje, lakini kumbe kwa ndani limeanza kuchakaa, na kwa kweli nilikuwa nahitaji nguvu kubwa, sasa leo nimeseme kweli wabunge saba wote waliopita hapa nikiwepo na mimi, tunaposema wengine hamna kitu nikiwepo na mimi,” alisema Kolimba.

Mbunge huyo wa zamani ambaye hivi sasa ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapindunzi wilayani Ludewa, alisema hayo kufuatia ahadi aliyoitoa mbunge wa sasa wa Ludewa, Deo Filikunjombe ya kuchangia shilingi milioni 50 kati ya shilingi milioni 75 zinazohitajika kwa ajili ya ujenzi wa kanisa jipya la katoliki kigango cha Manga kata ya Madilu.

Kanisa hilo ambalo limejengwa miaka ya 60 hivi sasa limepata ufa mkubwa na kuanza kuvuja kwenye paa zake, jambo ambalo limekuwa likisababisha hofu kwa waumini huenda likaanguka.

“Mimi nimefanya kazi ya ushirika, hapa kulikuwa na chama cha msingi, nimefanya ukaguzi miaka kenda (tisa), ni kawa mbunge na baadaye kuwa mkuu wa wilaya, sijawahi kupata milioni 50, hivyo ni kweli kabisa kutoa ni moyo siyo utajiri, Bwana Filikunjombe kwa kweli umenimaliza kabisa,” alisema Kolimba.

Aidha alisema  yeye akiwa mbunge wa Ludewa alikuwa akipita kwenye kata hiyo ya Madilu na kutoa msaada wa mifuko ya saruji kumi, wakati wa ujenzi wa sekondari ya kata hiyo.

“Nilileta mifuko kumi tu ya saruji wakati tunajenga sekondari, lazima tuseme ukweli hapa,  lakini leo Filikunjombe ametoa mifuko 200 ya saruji, ni kweli kabisa kazi anayoifanya mbunge Filikunjombe kwa sasa ni kubwa, sisi wabunge saba tuliopita hatujaweza kuifanya,” alisema Kolimba.
Mbunge huyo aliwaambia wananchi, “Hapa kweli hakuna mbunge mwingine yeyote aliyewahi kufanya makubwa kama haya, nilijitahidi mimi kidogo, tena kwa kuleta mifuko mitatu mitatu ya saruji, tunasema huyu Filikunjombe ni kiongozi wa watu. Tukubali kwamba mwenzetu ametushinda kwa kiwango kikubwa sana.”

Wabunge waliowahi kuongoza jimbo la Ludewa ni Violet Baraka aliyekuwa mbunge mwaka (1975 hadi 1980), John Simalenga, Mathias Kihaule (marehemu), Holace Kolimba (Marehemu), Chrispin Mponda (Marehemu), Stanley Kolimba, Profesa Raphael Mwalyosi na hivi sasa Deo Filikunjombe.

Katika hatua nyingine, Mbunge Filikunjombe akizungumza na wananchi wa kijiji cha Manga Kata ya Madilu wakati wa kukabidhi vifaa vya ujenzi mifuko 400 ya saruji, bati 200 na vioo pamoja na magodoro mawili, alisema ataendelea kuunga mkono jitihada za wananchi katika kuleta maendeleo kwenye wilaya ya Ludewa.

“Serikali yetu ya CCM inajenga shule kila kata, zahanati kila kijiji, nimekuja hapa kuwaunga mkono jitihada zenu wananchi, ningekuta hamjafanya kitu nisingeunga mkono,” alisema Filikunjombe.

“Nilikuja hapa nilikuta wenzangu mnao msiba wa maendeleo, na mimi nikasema nitalia, tukaenda kushuhudia kwa macho yangu kazi mnayoifanya, nawapongezeni sana,” aliwaambia wananchi hao.

Mbunge huyo aliwataka wananchi hao kuwasomesha watoto wao katika maeneo ambayo amekuwa akisaidia.

“Tusomeshe watoto, mimi nitakuwa mbunge hadi lini maisha yote, haiwezekani, itafika mahala nitasema sasa basi, wengine waendelee, nataka mchague mbunge atakayekuja aliyesoma sana,” alisema Filikunjombe.

Licha ya kuwa wananchi hao walimshawishi kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania mwaka 2015, lakini Filikunjombe alisema ubunge unamtosha kwani itakuwa rahisi kuwahudumia wananchi wake.

===mwisho==

No comments: