Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

October 21, 2013

CHUO CHA VETA CHA KWANZA MKOANI NJOMBE KATIKA WILAYA YA MAKETE CHAZINDULIWA.



Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dakt Jakaya Mrisho Kikwete akipata maelezo ya ujenzi wa chuo cha Veta wilayani Makete
 Wananchi wakimsikiliza Rais Kikwete
 Hili ni moja ya jengo la Veta wilayani Makete
  Rais kikwete akiweka jiwe la msingi katika chuo cha VETA wilayani Makete

Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Jakaya Mrisho Kikwete jana alizindua chuo cha VETA ikiwa ni chuo cha kwanza katika mpango wa Serikali wa kuhakikisha kila wilaya inakuwa na chuo cha ufundi staid ili kuhakikisha vijana wanapata fulsa ya ujuzi mbalimbali.

Akisoma taarifa ya ujenzi wa chuo hicho mkurugenzi mkuu wa VETA Tanzania Bw.Moshi katika ziara ya Rais katika wilaya za mkoa wa Njombe alisema chuo hicho kimejengwa kwa ushirikiano wa Halmashauri ya wilaya ya Makete na VETA taifa.

Alizitaja gharama za ujenzi wa chuo hicho hadi kukamilika ni shilingi 2.29 bilion ambapo alibainisha kuwa fedha taslimu ni shilingi 1.5 bilioni kwa ajili ya ujenzi na shilingi 785 milioni zilitumika kama gharama za vifaa.

Bw.Moshi alisema mchango wa Halmashauri ya wilaya ya Makete ni pamoja na  utengenezaji wa barabara ya kufika chuoni hapo,maji kwaajili ya ujenzi,umeme, mawe na mchanga pamoja na nyumba ya kuishi mafundi.

Alisema chuo hicho kimejengwa na wanafunzi pamoja na walimu wao kutoka chuo cha VETA Mpanda ambao wamefanya kazi kubwa wakishirikiana na wananchi katika kuhakikisha  ujenzi huo unakamilika mapema kwa muda uliopangwa.

“chuo hiki ni cha kwanza katika mpango wa Serikali wa kujenga vyuo vya VETA katika kila wilaya kati ya vyuo vingi kikiwemo chuo cha VETA wilayani Ludewa na kile cha Mkoa ambacho kitajengwa katika mji wa Njombe hivyo ni fulsa pakee kwa wananchi kupata kozi mbalimbali”,alisema Bw.Moshi.

Alizitaja changamoto zinazoikumba taasisi ya VETA ni pamoja na sheria ya manunuzi inayowataka kununua mitambo na vifaa vipya vya kujifunzia ambapo uwezo wa VETA kununua vifaa hivyo ni mdogo ukilinganisha na bajeti wanayoipata.

Bw.Moshi alisema katika somo la ufundi wa mitambo,magari na dege wanalazimika kununua injini mpya ili kuwawezesha wanafunzi kujifunzia hivyo alimuomba Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kuliomba Bunge la jamuhuri ya muungano wa Tanzania kulegeza masharti hayo yatakayowawezesha kutoa elimu kwa ufanisi zaidi.

Katika hotuba yake Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania  Dakt Jakaya Mrisho Kikwete alilipokea ombi hilo na kuahidi kulifanyia kazi kutokana na uzito wa jambo hilo linalorudisha nyuma juhudi za ufundishaji kwasababu ya masharti ya sheria ya manunuzi.

Dkt.Kikwete alisema mpango wa Serikali ni kuhakikisha kila wilaya inakuwa na chuo cha VETA ili kuhakikisha vijana wa kitanzania  wanapata fulsa ya kujiajili na kuajiliwa kwani elimu ndio msingi wa maisha ya mtanzania.

Katika ziara hiyo Dkt Kikwete licha ya kuzindua chuo cha VETA pia aliweza kuzindua zahanati,shule ya Sekondari Lupalilo yenye kidato cha tano na sita ambayo ilijengwa mwaka 1911 na kanisa la KKKT na kuwa shule ya kwanza wilayani Makete.

Dkt Kikwete aliwataka wananchi wilayani humo kuzitumia fulsa za elimu hasa katika kujiunga na masomo chuoni hapo ili kuweza kupata ujuzi wa kutengeneza vitu mbalimbali vinavyotokana na mazao ya miti na ufugaji wa ng’ombe wa maziwa.

Alisema wilaya ya Makete inaongoza kwa kilimo cha viazi hivyo ni jambo la msingi kama chuo hicho kitafundisha kozi zinazoendana na mazingira halisi ya mazao ya maeneo hayo baada ya kusafirisha viazi vibichi kwa kuvipeleka Dar es Salaam.

“Kwa ujenzi huu wa chuo cha VETA wilayani hapa ni ukombozi mkubwa kwa vijana wenu kwani wataweza kujifunza ufundi mbalimbali hasa katika kutengeneza samani kwa ni moja ya wilaya nchini inayozalisha mbao pia utengenezaji wa chipsi na kuziweka katika vifungashio na kuziuza nchini na nje ya nchi”,alisema Dkt Kikwete.

No comments: