Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

February 23, 2013

VIJIJI 19 WILAYANI LUDEWA VINATARAJIA KUNUFAIKA NA UMEME WA MAJI



Haya ndio maporomoko ya mto Lupali katika kijiji cha Njelela wilayani Ludewa yanayotarajia kuzalisha umeme utakao nufaisha vijiji 19
Viongozi wa shirika la LCBA na wataalamu wa upimaji wa Ardhi ili kupima eneo la kufunga mitambo
 Wajumbe wa shirika la LCBA wakiangalia ukubwa wa maporomoko ya mto Lupali
Mwandishi wa mtandao huu Nickson Mahundi akiwa na Bahati katika maporomoko ya mto Lupali katika kijiji cha Njelela
 Wataalamu wakiendelea na upimaji katika eneo la mradi wa umeme
Wataalamu wipima umbali kutoka mtoni
Mjumbe wa LCBA Bw.Donoto Mgeni maarufu kwa jina la Ndicheliwe akisaidia kusafisha mazingira kwaajili ya upimaji
Katibu wa shirika la LCBA Bw.Joseph Kayombo akiweka alama eneo la mradi
 maji ya mto Lupali
Alama zikiendelea kuwekwa
msitu unaotililisha maji katika mto Lupali
mambo ya vipimo yakiendelea mto Lupali
msitu wa mto Lupali

Mwandishi wa mtandao huu akiwa katika maporomoko ya mto Lupali

Wananchi waVijiji 19 wilayani Ludewa katika Mkoa wa Njombe wanatarajia kunufaika na huduma ya umeme utakao zalishwa na shirika lisilo la Serikali linalojihusisha na mambo mbalimbali ya kijamii la Ludewa Capacity Bulding Association(LCBA) lenye makao yake makuu Ludewa mjini.

Akiongea na waandishi wa habari katibu wa shirika hilo Bw.Joseph Kayombo alisema shirika lake linatarajia kuuzalisha umeme huo kupitia maporomoko ya Mto Lupali ulioko katika kijiji cha Njelela kata ya Mundindi wilayani Ludewa.

Bw.Kayombo alisema umeme huo unakadiliwa kutoa megawalt 30 ambazo zitavinufaisha vijiji 19 kwa gharama nafuu kutokana na shirika hilo kujihusisha na utoaji misaada na elimu katika maeneo mbalimbali ndani ya wilaya ya Ludewa.

Alivitaja vijiji vitakavyonufaika na huduma hiyo katika kata ya Mundindi kijiji cha Mundindi,Amani na Njelela,kata ya Ibumi ni kjiji cha Ibumi na Nyamalamba kata ya Madilu ni kijiji cha Madilu,Ilininda,Ilawa,Mfalasi na Manga kata ya Madope kijiji cha Madope,Luvuyo,Lusitu na Mangalanyene.

Vijiji vingine ni Mkongobaki,Lipangala,Ugela,Shaurimoyo na Mdilidili hata hivyo alisema umeme huo utakuwa na nguvu kubwa hivyo unaweza kusambaa katika vijiji vingi zaidi itakavyowezekana kutokana na wafadhiri wa mradi huo watakavyopendekeza.

“Tumeshafuata hatua zote za kisheria na REA wanatutambua hivyo wananchi wanapaswa kujenga nyumba nzuri za kudumu ili wajiandae na ujio wa neema hivyo ya umeme kwa kunavijiji tokea nchi hii ipate uhuru havijawahi sikia kama vinaweza kupata umeme hivyo wananchi watupe ushirikiano”,alisema Bw.Kayombo.

Diwani wa kata ya Mundindi kupitia chama cha Mapinduzi ambako umeme huo utazalishwa Bw.Vicent Mgina alisema amefurahishwa na jambo hilo kutokana na ukweli kwamba umeme ndio chachu ya maendeleo katika maeneo mbalimbali Duniani.

Bw.Mgina alisema wananchi wake kupitia umeme watapata fulsa ya kufanya biashara mbalimbali na kuanzisha viwanda vidogo vidogo ili kujipatia kipato kwa umeme huo utaenda sambamba na ujenzi wa chuo cha VETA katika kijiji cha Shaurimoyo hivyo watakaosoma chuo hicho wataweza kujiajiri kwa kuanzisha karakana zao.

Alisema kitu cha msingi kwa shirika hilo ni kufuata sheria za nchi na kuwashirikisha wananchi ili waweze kuona wao ni wenye mradi huo ili kuondoa migongano inayoweza kujitokeza kutokana na tamaduni za wananchi wa maeneo hayo kulima mabondeni katika vyanzo vya maji.

Aidha mjumbe wa shirika la LCBA Bw.Lazaro Mwinuka alifafanua kuwa shirika hilo unakadiliwakutumia  kiasi cha shilingi 40 Bilion kutoka Bank ya Dunia kupitia REA ambazo zitafanya kazi zote mpaka mradi huo utakapo kamilika.

Bw.Mwinuka alisema mchakato wa mradi huo umeshaanza lakini unatarajia kumamilika ifikapo mwaka 2014 kutokana na ukubwa wa mradi hivyo wananchi wa vijiji tajwa wanatakiwa kuanza maandalizi katika nyumba zao ili waweze kunufaika na mradi huo.

Hata hivyo Bw.Donota Mgeni maarufu kwa jina la Ndicheliwe mfanyabiashara wilayani Ludewa na mjumbe wa LCBA alisema wananchi wenye shughuri zao eneo la mradi watalipwa fidia zao mapema mwaka huu ili kupisha mradi huo.

Bw.Mgeni alisema kinachotakiwa kwa wananchi ni kutoa ushirikiano kwa viongozi wa vijiji na kata husika wanashirikishwa kwa kila jambo ili waweze kutambua manufaa ya umeme huo katika vijiji na kata zao na si vinginevyo.

Aliwataka kutokuwa na wasiwasi na shirka lao kutokana na wananchi hao kudanganywa na mashirka mengi yaliyowahi fika katika mapolomoko hayo na kuahidi yataweka umeme lakini hayakutimiza ahadi hizo na kutokomea kusikojulikana.

MWISHO.

No comments: