Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

April 08, 2014

WATUHUMIWA WA WIZI WA KUTUMIA SIRAHA KYELA WAFIKISHWA MAHAKAMANI.




WATUHUMIWA sita wa wizi wa kutumia siraha ambao ni Mashaka Juma(30) mkazi wa kyela kati,Issa Israel (gwalugwaja)(35) mkazi wa ndandalo,Juma Julius(mbwa mwitu)(31)mkazi wa Kajunjumele,Asedy Daud (41)mkazi wa bondeni,Musolini Mwamasinga (34) mkazi wa bondeni na Hasani Shindo (31) mkazi wa Kyela kati wamefikishwa katika mahakama ya wilaya ya Kyela mkoani Mbeya jana kujibu mashitaka yao yanayowakabili.

Kwa mujibu wa mwendesha mashitaka wa mahakama hiyo Nickolaus Tbba ni kuwa watuhumiwa hao wanakabiliwa na kesi tatu ya kwanza ni kuvunja nyumba kifungu cha 384 sura ya 16 ya kanuni ya adhabu iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002,kesi ya pili ni kuvunja nyumba na kuibakifungu cha 296 na kifungu cha 265 sura ya 16 ya kanuni ya adhabu na kesi ya tatu ni wizi wa kutumia siraha kifungu cha 287 A sura ya 16 ya kanuni ya adhabu.

Tbba alisema kuwa watuhumiwa hao walivunja na kuiba duka la Happy Kakusya na kuiba vitu mbalimbali vyenye thamani ya Tsh,million 1,duka lingine walilovunja ni la Pipi Yusuph ambapo watuhumiwa ni Mashaka Juma na Hasan Shindo na kuiba mali yenye Thamani ya Tsh,2,90,000 na kuwa vitendo hivyo vilifanyika tarehe 27 na 29 mwezi huu.

Aliitaja kesi ya tatu kuwa ni ya wizi wa kutumia silaha inayowahusu watuhumuwa sita kuwa kabla ya kuvunja na kuiba pesa Tsh,Mil, 1,pisi 60 za simu zenye thamani thamani ya Tsh,mil,2,na vitu vingine ambavyo jumla yake ni Tsh,Mil,5 na elfu 40,000 ambapo walimpiga na kumjeruhi na nondo kichwani mlinzi wa duka hilo Adam Mwankuga.

Katika tuhuma hizo washitakiwa wote waliyakana mashitaka hayo na wamerudishwa lumande hadi tarehe 16 mwezi huu kesi yao itakapotajwa tena chini ya Hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama ya wilaya Joseph Luambano.

Katika hatua nyingine Silvestar Mele (17) mkazi wa kitongoji cha Itunge wilayani hapa amefikishwa mahakamani akituhumiwa kumchoma kisi hadi utumbo kutoka nje Gwamaka mwamafupa siku ya tarehe 29 mwezi wa huu ambapo anashitakiwa kwa kifungu cha 225 sura ya16 ya kanuni ya adhabu iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002,mshitakiwa amekana shitaka na amerudishwa lumande hadi tarehe 16 mwezi huu kesi yake itakapotajwa tena.

Denis Mwaipaja (20)mkazi wa Kitongoji cha mikoroshoni amefikishwa katika mahakama hiyo kujibu tuhuma ya shambulio la haibu linalomkabili la kumkamata mwanamke na kumtomasa tomasa katika sehemu za mwili wake bila ridhaa yake siku ya tarehe 29 mwezi huu na ameshitakiwa kwa kifungu cha 1435 kifungu kidogo cha (1) na (2) sura ya 16 ya kanuni ya adhabu iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002 na amekana shitaka na yupo lumande baada ya kukosa mdhamini kesi itatajwa tena tarehe 16 mwezi huu.
Mwisho.

 Na Ibrahim Yassin,Kyela

No comments: