Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

March 25, 2014

FILIKUNJOMBE AENDESHA HARAMBEE YA UNUNUZI WA GARI LA PAROKIA WANANCHI WASEMA NI NURU YA KWELI.

 Mh.Deo Filikunjombe akifuatilia maelezo ya Kangi Lugola
 Deo Filikunjombe akionesha ushirikiano kwa kushikana mikono na Kangi Lugola baada ya kuchangia ununuzi wa gari la parokia ya kanisa Katoliki Ludewa mjini
 Mh.Kangi Lugola akiongea na waumini wa kanisa hilo
 waumini wa Kanisa katoliki ludewa mjiniwakimsikiliza mbunge wao Deo Filikunjombe
 katibu mwenezi wa CCM wilaya ya Ludewa Bw.Felix Haule akiongea na waumini wa kanisa hilo
 Katibu wa mbunge wa jimbo la Ludewa Bw.Stanley Gowele akiongea na waumini wa kanisa hilo

       Hizi ni baadhi ya fedha zilizochangwa na Deo filikunjombe katika halambee ya ununuzi wa gari.

MBUNGE wa jimbo la Ludewa katika Mkoa wa Njombe Deo Filikunjombe amefanikiwa kuchangisha papohapo jumla ya shilingi m.30.7 kati ya shilingi m.90 zinazotakiwa na kusakwa na waumini wa kanisa katoliki kwa ajili ya ununuzi wa gari la parokia ya Ludewa mjini.
 
Harambee hiyo ilifanyika machi mwaka huu katika kanisa la yesu kristu mkombozi lililopo Ludewa mjini ambapo ilifanyika misa maalumu kwa kuwashirikisha waumini kutoka vigango vyote vinyounda parokia hiyo ambavyo ni pamoja na Nyamapinda, Ludewa(K) na Ngalawale.
 
Ujio wa mbunge huyo ulikuja kufuatia mwaliko wa kamati ya ununuzi wa gari ambayo ilimtuma diwani wa kata ya Ludewa Monica Mchiro na mwenyekiti wa kamati hiyo mzee Kayombo kumwomba Filikunjombe kuja kuendesha harambee hiyo.

No comments: