Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

October 21, 2013

VIJIJI 19 WILAYANI LUDEWA VINATARAJIA KUFANYIWA UPEMBUZI YAKINIFU ILI KUWEZA KUNUFAIKA NA NISHATI YA UMEME




 Maporomoko ya mto Lupali katika kijiji cha Njelela wilayani Ludewa
 Misitu ya asili iliyoko kijiji cha Njelela
 Wajumbe wa shirika la LCBA wakiandaa mazingira ya upimaji wa maji ya mto Lupali
misitu ya mto Lupali

Mtaalamu wa upimaji Bw.Msumani akiendelea na upimaji wa maeneo ya mto Lupali
 
Shirika la Ludewa Capacity Bulding Association (LCBA) lenye makao yake makuu wilayani Ludewa mkoani Njombe kupitia wakala wa umeme vijijini(REA) linatarajia kufanya upembuzi yakinifu katika vijiji 19 ili kusambaza nishati ya umeme.

Akiongea na waandishi wa habari katibu wa shirika hilo Bw.Joseph Kayombo alisema shirika lake linatarajia kuuzalisha umeme huo kupitia maporomoko ya Mto Lupali ulioko katika kijiji cha Njelela kata ya Mundindi wilayani Ludewa na kusambaza vijiji 19.

Bw.Kayombo alisema kazi hiyo ya upembuzi yakinifu itafanyika kwa muda wa miezi sita ambapo tayari wataalamu kutoaka REA wameshavitembelea vijiji hivyo na kujiridhisha kutokana na andiko la kuomba fedha za kazi hiyo lililoandikwa na shirika lake.

 Akivitaja vijiji vitakavyofanyiwa upembuzi yakinifu na kunufaika na huduma hiyo ya umeme Bw.Kayombo alisema katika kata ya Mundindi kijiji cha Mundindi,Amani na Njelela,kata ya Ibumi ni kjiji cha Ibumi na Nyamalamba kata ya Madilu ni kijiji cha Madilu,Ilininda,Ilawa,Mfalasi na Manga kata ya Madope kijiji cha Madope,Luvuyo,Lusitu na Mangalanyene.

Vijiji vingine ni Mkongobaki,Lipangala,Ugela,Shaurimoyo na Mdilidili hata hivyo alisema umeme huo utakuwa na nguvu kubwa hivyo unaweza kusambaa katika vijiji vingi zaidi itakavyowezekana kutokana na wafadhiri wa mradi huo watakavyopendekeza.

Tumeshafuata hatua zote za kisheria na REA wanatutambua hivyo wananchi wanapaswa kujenga nyumba nzuri za kudumu ili wajiandae na ujio wa neema hivyo ya umeme hivyo kwa awali tunatarajia kufanya upembuzi yakinifu usiozidi miezi 6 ndipo ujenzi wa mitambo ya kuzalisha umeme na njia za umeme itafuata”,alisema Bw.Kayombo.

Diwani wa kata ya Mundindi kupitia chama cha Mapinduzi ambako umeme huo utazalishwa Bw.Vicent Mgina aliwataka wananchi wa vijiji hivyo kuwaunga mkono wataalamu watakao fanya kazi hiyo ya upembuzi yakinifi ili kuharakisha mchakato huo.

Mh.Mgina alisema wananchi wake kupitia umeme watapata fulsa ya kufanya biashara mbalimbali na kuanzisha viwanda vidogo vidogo ili kujipatia kipato kwa umeme huo utaenda sambamba na ujenzi wa chuo cha VETA katika kijiji cha Shaurimoyo hivyo watakaosoma chuo hicho wataweza kujiajiri kwa kuanzisha karakana zao.

 Aidha mjumbe wa shirika la LCBA Bw.Lazaro Mwinuka alifafanua kuwa shirika hilo unakadiliwakutumia  kiasi cha shilingi 92 Bilion kutoka Bank ya Dunia kupitia REA ambazo zitafanya kazi zote mpaka mradi huo utakapo kamilika.

Bw.Mwinuka alisema mchakato wa mradi huo umeshaanza lakini unatarajia kumamilika ifikapo mwaka 2014 kutokana na ukubwa wa mradi hivyo wananchi wa vijiji tajwa wanatakiwa kuanza maandalizi katika nyumba zao ili waweze kunufaika na mradi huo.

Alisema mpaka sasa ni kiasi cha shilingi 350 milioni ndicho kitakachotumika katika kazi za upembuzi yakinifu katika vijiji hivyo 19 ambapo fedha hizo ni kutoka kwa wakala wa umeme vijijini (REA)

Hata hivyo Bw.Donota Mgeni maarufu kwa jina la Ndicheliwe mfanyabiashara wilayani Ludewa na mjumbe wa LCBA alisema wananchi wenye shughuri zao eneo la mradi watalipwa fidia zao mapema mwaka huu ili kupisha mradi huo.

Bw.Mgeni alisema kinachotakiwa kwa wananchi ni kutoa ushirikiano kwa viongozi wa vijiji na kata husika wanashirikishwa kwa kila jambo ili waweze kutambua manufaa ya umeme huo katika vijiji na kata zao na si vinginevyo.

Aliwataka kutokuwa na wasiwasi na shirka lao kutokana na wananchi hao kudanganywa na mashirka mengi yaliyowahi fika katika mapolomoko hayo na kuahidi yataweka umeme lakini hayakutimiza ahadi hizo na kutokomea kusikojulikana.

MWISHO.



No comments: