Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

October 21, 2013

RAIS KIKWETE AWAHAKIKISHIA WANANCHI MKOANI NJOMBE UJENZI WA SOKO LA KIMATAIFA KATIKA MJI WA MAKAMBAKO.




 Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania akiwa amevishwa vazi la uchifu katika uzinduzi wa mkoa wa Njombe uliofanyika katika viwanja vya sabasaba mjini Njombe
 Waziri wa Elimu mh.Shukuru Kawambwa akihutubia wananchi mkoani Njombe
Mbunge wa jimbo la Ludewa Mh.Deo Filikunjombe akiwa na kitabu cha Njombe baada ya kukabidhiwa na Rais Kikwete
 Mama Salma Kikwete akiwasalimia wananchi wa Njombe katika uzinduzi wa mkoa huo
Rais akipata maelekezo jinsi kiwanda cha Chai Lupembe kilivyoanzishwa
 Wanafunzi wakiwa katika haraiki siku ya uzinduzi wa mkoa wa Njombe
Rais Kikwete akiwa na profesa Mwaliosi ambaye alikiandaa kitabu cha Njombe

Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete amewahakikishia wananchi mkoani Njombe ujenzi wa Soko la kimataifa katika mji wa Makambako ambao utaanza hivi karibuni ili kuweza kuwasaidia wananchi wa nyanda za juu kusini kufanya biashara za mazao yao katika hatua ya kimataifa.

Akikabidhi hati za ujenzi wa soko hilo kwa viongozi wa mji wa Makambako katika sherehe za uzinduzi wa mkoa wa Njombe jana Rais Kikwete alisema soko hilo ni la pili kujengwa nchini wakati jingine lilishajengwa mkoani Arusha ambalo limeonesha mafanikio makubwa kwa wafanyabiashara nchini.

Alisema mzinduzi wa mkoa wa Njombe uendane na kasi ya ukuaji wa maendeleo kwa wananchi ikiwemo ujenzi wa viwanda ambavyo vitawawezesha wananchi kusindika mazao yao na kuongeza bidii katika uzalishaji ambao utaenda sambamba katika bishara ya kimataifa ndani ya soko hilo.

Akizungumza katika sherehe za uzinduzi wa mkoa huo zilizofanyika jana katika viwanja vya sabasaba mkoani humo Rais Kikwete aliitaja mikoa ambayo inauwezo wa kuzalisha mazao mbalimbali ikiwemo ufugaji wa ng’ombe wa maziwani pamoja na mikoa ya Njombe,Mbeya,Rukwa,Iringa na Ruvuma ambayo itanufaika na soko hilo.

Alisema ifike wakati maziwa yasiagizwe nchi nyingine bali nchi jirani zinapaswa kuyanunua maziwa hayo nchini kwani kunauwezekano mkubwa katika maeneo ya Kituro wilayani Makete pakatumika kama sehemu mojawapo ya uzalishaji wa ng’ombe na kuwauzia wananchikwa bei rahisi ili waweze kufanya biashara ya maziwa kimataifa.

“Serikali itafanya kila linalowezekana ili kuhakikisha wananchi wa mkoa huu na mikoa yenye hali ya hewa nzuri kama hii ya Njombe  wameze kuwa wafugaji wa ng’ombe wa maziwa na kulima mazao yenye tija ambayo yatawawezesha kulitumia soko lao kwa ufanisi zaidi ili kujikwamua na ugumu wa maisha uliokithiri miongoni mwa wananchi”,alisema Rais.Kikwete.

Awali kabla ya kuzindua mkoa Rais Kikwete aliweza kufanya ziara ya kutembelea kata ya Lupembe mkoani humo ambapoaliweza k uzinduzia kiwanda cha kusindika majani ya chai kutokana na kata hiyo kutokua na kiwanda cha usindikaji wa majani hayo ya chai hali ambayo ilikuwa ikiwatesa wananchi wa eneo bilo.

Kiwanda hicho ambacho kimejengwa na mwekezaji kutoka nchini India kimekuwa mkombozi kutokana na wananchi wa maeneo ya kata ya Lupembe kutegemea zao hilo katika uchumi wao hali iliyokuwa ikiwalazimu kusafirisha chai hiyo hadi Njombe ili kupeleka kiwandani.

Kuhusiana na miradi ya maendeleo Rais Kikwete aliwasifu wananchi wa mkoa wa Njombe kwa kushirki kikamilifu katika kuleta maendeleo mkoani hapo kwani aliweza kujionea wananchi wanavyoweza kujishughurisha katika kujinasua katika wimbi la umaskini kwakufanyakazi zenye ufanisi kwa mwananchi mmoja mmoja.

Alisema Serikali imeona juhudi binafsi kwa wananchi hivyo watarajie kuungwa mkono na Serikali yao katika kila hatua ya maendeleo ikiwemo upande wa Afya,Elimu na Miundombinu kwani kwani upande wa mindombinu tayari barabara ya Njombe Lupembe imeshafanyiwa upembuzi yakinifu kwa ajiri ya ujenzi wa kiwango cha lami.

Alizitaja barabara nyingine ambazo zitajengwa kwa kiwango cha Lami katika mkoa wa Njombe ili kurahisiha bidhaa kuweza kufika haraka katika soko la kimataifa linalojengwa Makambako ni pamoja na barabara ya wilaya ya Makete ambayo itaweza kusafirisha mbao na mazao mengine .

Kuhusu barabara ya wilaya ya Ludewa alisema hilo halikwepeki kutokana na  wilaya hiyo kuwa na migodi mikubwa ya machimbo ya Makaa ya mawe Mchuchuma na  ujenzi wa kiwanda cha chuma Liganga inayatarajia kutekelezwa hivi karibuni na wawekezaji wa M.M.I na kampuni wan chi ya China.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete yuko mkoani Njombe katika ziara ya siku sita ambapo aliwasili mkoani humo Oktoba 17 mwaka huu ambapo ameweza kufanya kazi ya uzinduzi wa mkoa huo na baadhi ya miradi ya maendeleo na anatarajia kuzitembelea wilaya zote za mkoa huo na kuhitimisha ziara yake Oktoba 22 mwaka huu.

Mwisho.

No comments: