Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

October 20, 2013

AUAWA NA WANANCHI KWA KUPIGWA MAWE





Mkazi wa kitongoji cha Lamya Kijiji cha Mpunguti Kata ya Katumbasongwe Wilayani Kyela Mbeya Godfrey Mwamwenda (20) amefariki dunia kwa kupigwa na wananchi wenye hasira kali baada ya kutuhumiwa kuiba Ng:ombe katika Kijiji cha Lupembe Kata ya Ikolo Wilayani hapa.

Akizungumza na Tanzania Daima leo (jana) Afisa mtendaji wa Kijiji cha mpunguti Kata ya Katumbasongwe Lusajo Mwakapiso alisema tukio hilo lilitokea saa mbili usiku wa kuamkia leo baada ya mashuhuda kumuona akisafirisha ng”ombe huyo nyakati za usiku na ndipo walipomtilia shaka na kuanza kumdadisi.

Alisema walifikia hatua hiyo ya kumuuliza kuhusu uhalali wa Ng:ombe huyo baada ya kusikia kuwa kuna Ng”ombe kaibiwa na ndipo walipopiga mayowe ya kuashiria mwizi na kuwa baada ya mayowe hayo wananchi walifika kwa wingi na kuanza kushambulia kwa fimbo na mawe hali iliyopeleke kufariki dunia papo hapo.

Aliongeza kuwa baada ya kutokea tukio hilo walilijurisha jeshi la Polisi ambao walifika katika eneo hilo na kuuchukua mwili huo na kuupeleka katika hospitali ya Wilaya ya Kyela kwa uchunguzi zaidi.

Ndugu wa karibu  na marehemu huyo ambaye hakutaka jina lake litajwe alisema kuwa Kijana huyo ambaye alikuwa akisoma shule ya sekondari ya Ikolo aliacha shule akiwa kidato cha pili na kuwa alianza vitendo hivyo katika familia yake ambapo katika siku za nyuma aliwahi kuiba Ng:ombe wa baba yake aliyemzaa.

Katika hatua nyingine Mkazi wa kitongoji cha Mwakikome kijiji cha Mpunguti kata ya Katumba songwe Wilayani hapa Julius Mwambelo (38) amefarika dunia baada ya kugongwa na gari katika barabara itokayo Kyela kwenda Katumba songwe.

Kwa mujibu wa afisa Mtendaji wa Kijiji hicho Lusajo Mwakapiso ni kuwa tukio hilo limetokea leo saa 5 hasubuhi wakati mtu huyo akivuka barabara na ndipo gari hilo aina ya Center lenye namba za usajili T.318 BHY lililokuwa limebeba mtumbwi likitokea kyela mjini kuelekea Katumba songwe likipeleka mtumbwi katika ziwa nyasa.

Mashuhuda waliokuwepo katika eneo hilo la ajali hiyo walisema kuwa chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi wa dereva na kuwa alionekana kushindwa kulimudu gari hilo kutokana na vumbi iliyotanda katika barabara hiyo.

Mganga wa zamu aliyekuwepo katika hospitali ya Wilaya ya kyela Dk.Nsubili Mwansule mbali na kukiri kupokea miili hiyo pia alisema kuwa mtu huyo aliyegongwa na gari alifariki dunia baada ya kuumia huku damu ikivuja ndani kwa ndani,na aliyepigwa kwa wizi alikua ameumizwa vibaya katika sehemu kadhaa katika mwili wakekutokana na kipigo hali iliyopelekea kifo chake.

Jeshi la polisi Wilayani Kyela limedhibitisha kuwepo kwa matukio hayo na kuziruhusu failia hizo kuendelea na taratibu za mazishi huku wao wakiendelea na uchunguzi.
Mwisho.
 Na Ibrahim Yassin,Kyela

No comments: