Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

September 30, 2013

OPERESHENI SANGARA YA CHADEMA YAISAMBARATISHA NGOME YA MWAMBARASHWA.



CHAMA Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kupitia operesheni sangala kimebomoa Ngome ya Mbunge wa Rupa Victor Mwambalaswa kwa kunyakuwa wanachama zaidi ya 9000 huku walio wengi wakiwa ni wafuasi wa chama cha Mapinduzi (CCM).

Akizungumza na waandishi wa habari jana Wilayani humo Mkufunzi wa chama hicho kanda nyanda za juu kusini Christopher Mwamsiku alisema kuwa katika operesheni ambayo wameifanya kwa wiki tatu hadi kufikia jumatani ya wiki iliyopita tayari wamekusanya wanachama wapya 8000 kutoka jimboni kwa mbunge Mwambalaswa.

Mwamsiku alisema kuwa katika operesheni hiyo wamezunguka katika vijiji vya na kujikusanyia wanachama wapya kwenye mabano ni Kijiji cha Mpela kata ya Kambikatoto (68), Kambi katoto (108), Bitimanyanga (260) kata ya Mafyeko (400), Isangambi (300), Matwiga (600), Mtanila (140), Igangwe (200), na Luwalanje (150).

Aliongeza kuwa vijiji vingine ni pamoja na Makongolosi (2000), Mwaoga (60) Matundasi (1200), Itewe (28) Mamba (140) Upendo (300) Mamba A (130) na kubainisha kuwa taarifa zingine zilikuwa bado hazijakamilika ili waweze kuzitoa kwa vyombo vya Habari.

Akizungumzia sababu za wananchi hao kuhamia kwenye chama hicho Mwamsiku alisema kuwa hiyo inatokana na wananchi kuchoshwa na manyanyaso wanayofanyiwa na serikali iliyopo madarakati hasa jamii ya wafugaji ambao ndio wamekuwa chambo cha mapato kwa Halmashauri ya Chunya.

Alisema wananchi wengi wametua shutuma zao kwa viongozi wa vijiji ambao wengi wao ni wanachama wa CCM ambao wamekuwa wakiwatoza shilingi 200,000 za kitanzania ili waweze kuhamia vijiji vingine wakitokea  Mikoa ya Shinyanga, Tabora na maeneo ya Igunga.

Aliongeza kuwa jamii ya wafugaji wameonekana kama vile sio watanzania tena bali ni kama wakimbizi na ndio maana walipo waeleza haki zao waliweza kuitikia wito wakujiunga na chama ambacho kinapigania haki za wananchi.

Alitoa mfano kuwa wabunge wa CCM wamekuwepo katika jimbo la Rupa kwa miaka nenda rudi lakini wameshindwa kuwajengea watoto shule ya sekondari katika kata ya  Kambi katoto haina hata shule moja ya sekondari huku ikiwa na shule ya msingi moja tu jambo ambalo linasababisha watoto kutembea umbali wa kilomita zaidi ya 15.

Alisema kuwa kutokana na umbali huo wananchi wamekuwa wakikata tama kuwapeleka watoto shuleni jambo ambalo linasababisha kujikita zaidi kwenye ufagaji badala ya kujiendeleza na elimu.

Kwa upande wake Mkuu wa msafara wa operesheni hiyo Peter Edward alisema kuwa jimbo hilo limekuwa na idadi kubwa ya watoto kutokana kuwepo shule chache hivyo kusababisha watoto wengi kujiingiza kwenye machimbo ya dhahabu na kisha kuzaliana ovyo.

Edward alisema kuwa uongozi wa Wilaya hiyo pamoja na Mbunge wao hawana huruma na makabira ya Wasukuma na Wamang’ati ambao ndio wahanga kutokana na kuwatumia kama ndio vitega uchumi vya halmashauri kutokana na kumiliki mifugo mingi hivyo kuiingizia Halmashauri pesa nyingi.

Kiongozi huyo wa msafara aliwataka viongozi hao kuwaheshimu wafugaji kwa kuwapa haki zate stahiki kwa kuwa na wao ni sehemu ya wananchi wa Tanzania na si kama wanavyofanyiwa kana kwamba wao hawana haki katika nchi yao.

MWISHO.
Na Ibrahim Yassin, Chunya

No comments: