Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

September 11, 2013

WAKULIMA WA MAHINDI WILAYANI LUDEWA WALALAMIKIA UCHELEWESHAJI WA MALIPO YAO.

 

Bi.Rose Mbuya  msimamizi wa NFRA kituo cha Ludewa mjini akiwa kazini
 Bi.Rose Mbuya akiendelea na majukumu ya kila siku
            Baadhi ya mahindi ambayo yameshanunuliwa

Wakulima wilayani Ludewa katika mkoa wa Njombe wameanza kutoa malalamiko kutokana na kutolipwa fedha zao kwa wakati kutoka kwa wakala wa hifadhi ya chakula Taifa(Nation Food Reseve Agents)kwani mategemeo yao ni kuuza mahindi na kupata fedha kwa wakati ili waweze kuwalipia watoto wao michango ya shule.

Akitoa malalamiko hayo mmoja mmoja wa wakulima wilayani hapa Bw.Mathayo Mwinuka alisema kuwa kumekuwa na ucheleweshaji mkubwa wa malipo tofauti na awali ambapo ilikuwa haidizi muda wa wiki moja baada ya kupima mahindi na kupewa fundi wakulima kulipwa fedha zao.

Bw.Mwinuka alilalamikia hilo kutokana na mamlaka hiyo inayonunua mahindi wilayani Ludewa na wilaya nyingine nchini kukaa na fedha za wakulima wa mahindi wilayani humo zaidi ya wiki tatu hivi sasa bila ya kuwalipa wakulima hao ambao hutegemea fedha hiyo katika kulipia ada watoto wao na matumizi ya kila siku.

“Inashangaza kuona tunauza mahindi ili tuweze kutatua matatizo yetu haraka lakini tunacheleweshewa malipo yetu mpaka watoto wetu wanafukuzwa mashuleni na kuzuiliwa kufanya mitihani kutokana na kukosa ada,kwani awali tulikuwa tukiuza mahindi na kupata fedha kwa wakati hivyo tunaomba Serikali kuliangalia hilo sisi si wakulima wa kahawa ambao huchukua fedha kwa msimu”,alisema Bw.Mwinuka.

Alisema mpaka sasa ni wananchi wengi ambao wameuza mahindi yao katika mamlaka hiyo hawajapata fedha lakini wako wengine waliowauzia walanguzi tayari wameshalipwa fedha zao kwa wakati hali inayowakatisha tamaa wakulima wengine kupeleka mahindi katika mamlaka hiyo wakihofia kucheleweshewa fedha zao.

Aidha Msimamizi wa manunuzi wa mamlaka ya NFRA katika kituo cha Ludewa mjini Bi.Rose Mbuya aliwataka wakulima hao wasiwe nawasiwasi kuhusiana na malipo ya mazao yao kwani kulikuwa na matatizo kidogo katika ofisi ya kanda Makambako lakini tatizo hilo limesha tatulika na hivi punde malipo hayo yatafanyika.

Bi.Mbuya alisema mpaka sasa mahindi yaliyonunuliwa ni zaidi ya tani 64501 na bado mahindi yanaendelea kununuliwa hivyo wakulima wanashauliwa kuendelea kupeleka mahindi yao ili yapimwe mapema bila kujali fedha za awali bado hazijalipwa kama wanavyolalamika.

Alisema kuwa wamepokea malalamiko mengi yakiwemo ya kutotenda haki katika upimaji na wengine kukataa kukatwa kiasi kilo moja na nusu kwaajili ya uchafu wa mahindi wanayoyaleta,hizo zote ni changamoto tu lakini malipo yao yatafanyika hivi karibuni.

“ni kweli wakulima hawajalipwa kwa muda mrefu na tunakili tumewaharibia malengo yao lakini wasihofu walipo yatafanyika ila kitu cha msingi ni kwamba wasikatishwe tamaa na hali hii iliyotokea sasa,kulikuwa na matatizo kidogo katika kituo cha Makambako ila hali imeshatengamaa nawashauri waendelee kuleta mahindi yao malipo yatafanyika”,alisema Bi.Mbuya.

Bi.Mbuya alisema wanakumbana na changamoto nyingi katika manunuzi ya mahindi ikiwemo ya wakulima kuleta mahindi machafu yenye fumbi na kugomea wanapopewa utaratibu wa kufanya kutokana na hali hiyo imekuwa vigumu kuwaelimisha wakulima hao kutokana na wao kuona hawatendewi haki.

Mwisho.
habari hii ni kwa udhamini wa Lukotiko bucher.

Ni wauzaji wa nyama ya Ng'ombe wa kienyeji wanapatikana wilayani Ludewa.
ufikapo wilayani Ludewa wanapatikana sokoni katika jengo la soko la Samaki.

kwa nyama bora kwaajili ya harusi,sherehe na matatizo mbalimbali onana na Lukotiko bucher.

Pia wananunua ng'ombe wa kienyeji pahala popote wilayani Ludewa.

kwa mawasiliano zaidi piga simu namba 0765878297/0764096248/0765796655 na 0755194056.
kutana na Lukotiko Bucher kwa nyama bora.

No comments: