Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

September 11, 2013

MWALIMU AFUNGWA MIAKA 30 KWA KUBAKA NA KUMLAWITI KINYUME NA MAUMBILE MWANAFUNZI WAKE.




MAHAKAMA ya Wilaya ya Ludewa katika Mkoa wa Njombe imemhukumu kwenda jela miaka thelathini na kuchapwa viboko 30 matakoni mwalimu Romanus Msango wa shule ya msingi Ingwachanya na mkazi wa Lupembe wilayani Njombe kwa kosa la kubaka mwanafunzi wa miaka 14 na kumuumiza vibaya katika sehemu za mwili wake.

Akisoma hukumu hakimu mkazi mfawidhi katika mahakama ya wilaya ya Ludewa Fredrick Lukuna alisema mahakama imeridhika na ushahidi uliotolewa na upande wa mashtaka na kwamba hakuna shaka lolote katika kuthitisha mshtakiwa kutenda kosa hilo linaloangukia katika kifungu namba 1309(1) na 31(1) kaanuni ya adhabu zuzu ya mwaka 2002.

“””” pamoja na kuwa mshtakiwa ni mkosaji wa kwanza na kwa kuzingatia taaluma ya mshtakiwa na makosa haya kushamili katika jamii ya wana Ludewa, matendo haya yakiachwa yanaweza kuleta athari kwa watoto na wananwake ikiwemo magonjwa ya kuambukizwa. Natoa amri utakwenda jela miaka 30 na viboko thelethini.””” aliamuru Lukuna

Awali ilidaiwa mahakamani hapo na mwendesha mashtaka mratibu wa polisi Edison Kasekwa(SP) kuwa mshtakiwa Romanus Msango alitenda ukatili huo wa kinyama Augost 20 mwaka jana katika kijiji cha Masimbwe kata ya Mlangali ambapo kabla ya kutenda kosa hilo alimshambulia mhanga na kisha kubaka na kumlawiti na kumsababishia maumivu makali mwilini.

‘’’’’’ hakuna makosa ya awali kwa mshtakiwa hata hivyo serikali ilimpa dhamana kubwa ya kulea watoto ambao ni nguvukazi ya Taifa la kesho lakini amewageuka na kutenda kitendo kinyume na maadili ya kazi yake na kuidharirisha taaluma pamoja na serikali naomba mahakama itoe adhabu kali ili liwe fundisho kwa walimu wenye tabia kama hii’’’’’ alihitimisha Kasekwa

Kasekwa aliongeza kuwa mshtakiwa alikusudia kutenda makosa hayo kwa sababu alimfuata mwanafunzi huyo shambani alikokuwa akivuna mahindi na wenzake ambao walikimbia kwenda kijiji kutoa taarifa baada ya mwalimu kumkamata mwenzao na kumpeleka kichakani.

Wakati huohuo watu wawili Bahati Mtega na Flowin Mtweve wakazi wa Milo wamehukumiwa kifungo cha maisha na kuchapwa viboko 12 kila mmoja kwa kosa la kumbaka kwa pamoja mtungo au (gang rape) Ester Mchiro makosa yanayoangukia katika kifungu cha 131(A).

Watuhumiwa hao walimbaka Bi. Ester Mchiro ambaye ni mke wa mtu hali ambayo ilisababisha mama huyo kupiga kelele na kuomba msaada ndipo raia wema walipokusanyika na kumkamata moja wa wabakaji hao na kumshikisha adabu kabla ya kumpeleka kituo cha Polisi Lugarawa ambapo mtuhumiwa mmoja alitimua mbio.









No comments: