Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

September 29, 2013

MASHINDANO YA DRAFTI WILAYANI KYELA YASHIKA KASI



MASHINDANO ya Ligi ya Pambana Saidia Jamii  kumtafuta Bingwa wa Wilaya katika mchezo wa Drafti Wilayani Kyela Mkoani Mbeya yamefikia tamati jana huku Oboti Mwakasungu akiibuka mshindi wa mashindano hayo na kujinyakulia Mbuzi jike mwenye uza uzito,

Ligi hiyo iliyoshirikisha wachezaji 42 kutoka katika timu za Tarafa zote mbili Unyakyusa na Ntebela ambayo ilianza kwa njia ya makundi na baadaye mtoano na jana ilikuwa ni fainali ya mwisho na kupatikana washindi wane ambao walikabidhiwa zawadi zao.

Katibu wa Chama cha Drafti Wilayani Kyela Jamesi Mwambungu aliwataja washindi hao kuwa ni Obote Mwakasungu aliyeshika nafasi ya Kwanza aliyepata Mbuzi Mwenye Thamani ya Tsh,100.000,wapili alikuwa ni Willy Mwambete aliyepata Kuku wanne jogoo wenye thamani ya 48,000,wa tatu ni Hamis Chengula aliyejipatia kuku watatu tetea wenye thamani ya Tsh 30,000,na wane alikuwa ni Ibrahim Mwakanyamale aliyeambulia kuku wa wili tetea wenye thamani ya Tsh,20.000.

Mwambungu pia alitoa zawadi kwa waendeshaji wawili wa ligi hiyo ambao ni Peter Senge na Danny Mwakila ambao walipewa shilingi elfu 4,000, kwa kila mmoja.

Mwenyekiti wa Chama hicho Gasper Mwasimba aliwapongeza washindi hao kwa kuibuka na ushindi na kuwataka wachezaji wengine kujitokeza kujiunga na mchezo huo ili waweze kushiriki mashindano mengine pindi yatakapo anza.

Mshindi wa mashindano hayo Obote Mwakasungu alisema kuwa hakutegemea kama ataibuka na ushindi kwakuwa ligi hiyo ilichezwa na wachezaji wenye uzoefu hivyo anajisikia furaha yeye kuibuka na ushindi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Asas ya Pambana Saidia jamii Taifa ambaye ndiye aliyedhamini wa mashindano hayo Abraham Mwanyamaki alipongeza jitihada zilizofanya na viongozi hao waliofanikisha mchezo huo na kwamba ataendelea kutoa mchango wake pale utakapohitajika ili kusaidia kukuza mchezo huo.

Alisema kuwa Ligi ijayo ataboresha zawadi ili kuwavuta vijana wengi  wajiunge na mchezo huo kwa lengo la kupata fursa ya kuonesha vipaji vyao katika mchezo huo unaotambulika kimataifa.
Mwisho.
 Na Ibrahim Yassin,Kyela

No comments: