Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

September 30, 2013

DC LUDEWA AZITAKA TAASISI ZA DINI KUHUBIRI AMANI NCHINI









Mkuu wa wilaya ya Ludewa katika mkoa wa Njombe Bw.Juma Solomon Madaha amezitaka taasisi za Dini nchini kuhubiri amani kwa waumini kwani kwa kufanya hivyo kutapunguza migogoro ya kidini inayoweza kujitokeza kutokana na kutovumiliana.

Bw.Madaha aliyasema hayo jana wakati akifunga mkutano wa Injili katika kanisa la Anglikana mtaa wa Ludewa mjini,mkutano huo uliwakutanisha wahubiri mbalimbali wa kutoka mikoa ya Njombe,Mbeya na Mtwara.

Alisema kutokana na vurugu za chinichini zinatoendelea nchini ambazo ni pamoja na kumwagiwa tindikali kwa viongozi wa Dini na uchoamaji wa nyumba za ibada unaoendelea ni vema taasisi za kidini zikahubiri amani ili waumini waweze kumrudia Mungu.

Bw.Madaha alisema kumekuwa na vurugu za chinichini zinazochochea udini hali ambayo haina tija ndani ya Taifa la Tanzania hivyo waumini wa Dini zote wanapaswa kuwapuuza wachochezi na wenye lengo la kuwagawa watanzania kwani hawana nia nzuri na watanzania wenye tabia ya utulivu.

waasisi wa taifa hili yaani Baba wa taifa Mwalimu Nyerere na Shekh.Karume walisisitiza amani kwa watanzania hivyo nawaomba wahubiri wote liombeeni taifa letu liwe na amani na waumini wa Dini zote wawe na moyo wa kuvumiliana kwani hakuna aliye mkamilifu hapa duniani”,alisema Bw.Madaha.

Bw.Madaha aliyema Serikali iko bega kwa bega na kazi nzuri zinazofanywa na Dini zote katika kulijenga taifa hivyo kila muumini wa Dini yoyote anatakiwa kuhakikisha amani inaendelea kudumishwa kama ilivyozoeleka kwa watanzania.

No comments: