Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

August 19, 2013

DAKTARI KORTINI KWA KUGUSHI NA KUISABABISHI SERIKALI HASARA




ALIYEKUWA mratibu wa Bima ya Afya katika Hospitali ya wilaya ya Ludewa Mkoani Njombe Daktari Adamson Ndapisi amefikishwa katika mahakamani ya Hakimu mkazi kwa makosa tisa ikiwemo kugushi barua na saini za watumishi wenzake na kujipatia jumla ya shilingi m.3.3 mali ya serikali.

Mbele ya hakimu mkazi mfawidhi katika mahakama ya wilaya ya Ludewa Fredrick Lukuna mwendesha mashtaka wa taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa (TAKUKURU) mkoa wa Njombe Richard Marekani akaiambia mahakama kuwa mshtakiwa Adamson Ndapisi alitenda makosa hayo aprili 2008 akiwa mratibu wa bima ya afya wilaya.

Katika shtaka la kwanza marekani akaiambia mahakama kuwa mshtakiwa aligushi barua ya kuomba shilingi m.3.3 kwa Halmashauri ya wilaya ya Ludewa kwa lengo la kuendesha semina hewa kwa watumishi wa idara ya Afyahuku akijua ni uongo chini ya kifungu 333, 335,(d) 1 kanuni ya adhabu sura ya 16.

Makosa mengine ni matumizi mabaya ya madaraka chini ya kifungu 22 kanuni ya adhabu ya sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa namba 11 ya mwaka 2002 ambapo mshtakiwa anatajwa kughushi risiti yenye thamani ya jumla ya shilingi milioni 2.1 na kuwasainisha watumishi wa idara ya afya huku akitambua kuwa ni kosa.

Aidha mfanyabiashara maarufu wa mgahawa wa NAM CAFE ulioko mjini Ludewa Maria Haule ambaye katika kesi hiyo ni mshtakiwa wa pili anakabiliwa na kosa moja la kushiriki kuidanganya serikali kwa kutoa risiti za vyakula hewa zinazoonesha kuwa mshtakiwa alinunua vitu dukani kwake kosa linaloangukia katika fungu la namba 30 ya sheria ya kuzuai na kupambana na rushwa namba 11 ya mwaka 2007.

Washtakiwa wote walikana kuhusika na makosa yanayowakabili, na kesi imeahirishwa hadi agosti 19 mwaka huu kesi itakapokuja kusikilizwa kwa awali.washtakiwa wote waliachiwa baada ya kutimiza masharti ya dhamana ambapo kila mmoja alitakiwa kuwa na wadhamini wawili wenye mali isiyohamishika isiyopungua thamani ya shilingi milioni sita.

mwisho
 Na Bazil Makungu Ludewa

No comments: