Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

July 19, 2013

WANANCHI WA KIJIJI CHA LUDENDE WILAYANI LUDEWA WAJITOLEA KUCHIMBA BARABARA


.
 wananchi wa kijiji cha Ludende wakiwa katika shughuri ya uchimbaji wa barabara






aliyetangulia mbele ni Afisa mtendaji wa kijiji cha Ludende wakihamasisha wananchi katika shughuri ya uchimbaji barabara



WANANCHI wa kijiji cha Ludende kata ya Ludende wilayani Ludewa katika mkoa wa Njombe wameamua kuchimba barabara itakayo wasaidia kusafirisha mazao yao kutoka kijijini hapo na kuyapeleka sokoni ili kukwepa mlima katika barabara ya awali ambayo walitumia gharama kubwa wakati wa kukodi vyombo vya moto.

Uchimbaji wa barabara hiyo umekuja baada ya barabara waliyokuwa wakiitumia kuwa na mlima mkali hali ambayo ilikuwa ikisababisha gari za mizigo kushindwa kupanda mlima huo zikiwa na mzigo na kusababisha gharama kubwa ya usafirishaji wa mazao.

Akizungumza jana Mwenyekiti wa kijiji cha Ludende Bw.Samwel Shagama alisema ni kwa muda mrefu kijiji hicho kimekuwa kisiwani kutokana na barabara hiyo kuwa na mlima mkali hivyo wananchi wameamua kujitolea kwa nguvu zao ili kuchepusha barabara hiyo.

Bw.Shagama alisema licha ya gharama za usafirishaji wa mazao pia hata gharama za kukodi bodaboda kutoka kijijini hapo na kupeleka wagonjwa katika kijiji cha jirani cha Milo ambako kuna Hospitari kubwa hali ilikuwa vivyo hivyo.

uanzishwa wa barabar hii inayounganisha kijiji cha Ludende kwena kata ya Milo hadi barabara ya Kigasi ni ukombozi mkubwa kwani tumekuwa tukinyanyasika mno kwa bei kubwa hasa kwa wamiliki wa vyombo nya moto”,alisema Bw.Shagama.

Alisema kutokana na manyanyaso hayo wananchi kwa umoja wao na kwa hiari yao waliamua kufanya utafiti wapi barabara hiyo itapita na kufikia muafaka ambao umepelekea kuichimba barabara hiyo haraka bila ya kuomba msaada Serikalini.

Aidha afisa mtendaji wa kijiji hicho Bw.Timoth Mwinuka alisema barabara hiyo iliyochimbwa na wananchi ni nyembamba hivyo inahitajika upanuzi kwa kutumia mashine.

Bw.Mwinuka alisema suala la upanuzi ili kuwaungamkono wananchi wa kijiji cha Ludende atalifikisha katika ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Ludewa kwani barabara hiyo ni kubwa ambayo inaunganisha zaidi ya kata nne.

Alikubali kuwa awali wananchi wakijiji hicho walishindwa kusafirisha mazao yao bamoja na wagonjwa pindi inapotokea dharula kutokana na barabara ya awali kuwa na mlima mkali ambao ulikuwa hatari zaidi lakini kwa kuchepucha katika kuukwepa mlima huo imekuwa nafuu zaidi.

Bw.Mwinuka aliwataka wananchi wa kijiji cha Ludende na vijiji jirani kuitunza barabara hiyo kwa kutopitisha mifugo ili siku wakifika wataalamu kutoka Serikalini kwaajili ya kuikagua waikute ikiwa katika hali nzuri.

Mwisho.

No comments: