Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

July 02, 2013

LUDEWA YATUMIA 1.3 KATIKA MIRADI YA MAENDELEO


 Afisa utumishi wilaya ya Ludewa Bw.Horace Kolimba akihutubia wananchi

 Mwenyekiti mstaafu wa halmashauri ya wilaya ya Ludewa Mzee Hilaly Nkwera akiwasalimia wananchi
Burudani ya ngoma ya mganda ya kikundi cha mzalendo ikiendelea kuburudisha

vijana wakijiandaa katika shindano la kunywa soda
 Afisa maendeleo ya jamii wa wilaya ya Ludewa Bw.Malima akitoa mkono wa pongezi kwa mshindi wa shin dalo la kukimbiza kuku
Afisa utumishi Horace Kolimba akisoma taarifa ya halmashauri ya wilaya ya Ludewa

Kaimu mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Ludewa Bi.Mwano aliyesimama katikati akijiandaa kupokea maandamano ya wafanyakazi wa Serikali za Mitaa


 Mwanasheria wa halmashauri ya wilaya ya Ludewa Bw.Chalamila aliyetangulia akifuatiwa na Hakimu wa wilaya ya Ludewa Mh.Lukuna



kikundi cha ngoma ya ngwaya kikijiandaa kutumbuiza
HALMASHAURI ya wilaya ya Ludewa Mkoani Njombe, katika kipindi cha julai 2012 hadi juni 30, 2013 imetumia jumla ya shilingi 1.3bilioni katika shilingi 3.3bilioni zilizokisiwa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo fedha iliyotolewa na serikali pamoja na wahisani mbalimbali.

Taarifa hiyo ilitolewa jana katika kilele cha maadhimisho ya siku ya serikali za mitaa iliyofanyika julai mosi mwaka huu katika uwanja wa mpira wa miguu Ludewa mjini ambapo pamoja na mambo mengine halmashauri ilitoa ufafanuzi wa mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha wa 2012/2013.

Akitoa taarifa kwa wananchi kwa niaba ya Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Ludewa, afisa utumishi na utawala Horace Kolimba alisema kuwa maadimisho haya yanafanyika katika kila ngazi kuanzia Taifa,Mkoa,Wilaya, Kata, Kijiji hadi kitongoji na kwa upande wa Ludewa maadhimisho yameenda sanjari na shughuli za ujenzi wa Taifa yakiwemo maonesho,burudani na hotuba kutoka kwa viongozi.

No comments: