Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

July 23, 2013

ASKOFU SIMALENGA RUKSA KULIGAWA JIMBO LA NJOMBE NA KUANZISHA JIMBO JIPYA LUDEWA.



Askofu Ssimalenga akifungua mkutano katika kanisa la Anglikana wilayani Ludewa
Mwnyekiti wa taskforce Mh.Edward Haule ambaye pia diwani wa kata ya Ibumi akimpa mkono wa shukrani Askofu Simalenga












 Askofu Simalenga akiwa na kamati maalumu(task force)ambayo inaandaa mchakato wa uanzishwaji wa Dayosisi mpya itakayotambulika kwa jina la Mount Living stone


KANISA Anglikana Dayosisi ya Kusini Magharibi mwa Tanganyika jimbo la Njombe limeanza mchakato wa kuligawa jimbo hilo na kuunda Dayosisi mpya ya Mount Livingstone itakayokuwa na makao yake makuu wilayani Ludewa.

Akizungumza jana katika uzinduzi wa kamati maalum(task force) inayoratibu kuanzishwa kwa doyasisi mpya itakayopewa jina la Mount Livingstone Askofu mkuu wa Dayosisi ya kusini magharibi mwa Tanganyika jimbo la Njombe John Simalenga alisema sababu ya kuligawanya jimbo ni kutokana na ukubwa wa jimbo lililopo.

Askofu Simalenga alisema lengo kuu la kuanzishwa kwa Dayosisi ya Mount Livingstone itakayokuwa na makao yake makuu mjini Ludewa ni kusogeza huduma za kimwili na kiroho karibu na watu kufuatia dayosisi ya kusini magharibi mwa Tanganyika kuwa na eneo kubwa,jambo linaloongeza mzigo mkubwa katika kutoa huduma.

Aidha aliwataka washiriki katika mchakato huo kuongozwa na roho mtakatifu kwa kujawa na hekima, uzalendo upendo na busara ili kufanikisha zoezi hilo gumu na kulitaja eneo linalomilikiwa na Dayosisi yake kuwa ni pamoja na eneo lote la wilaya ya Ludewa, Makete, Njombe, Mufindi katika mkoa wa Iringa na Mlimba katika mkoa wa Morogoro.

Simalenga alisema kutokana na mzigo ambao Dayosisi anayoisimamia kuwa mkubwa imelazimu kuanzisha Dayosisi nyingine ili kuwasogezea waamini huduma ya kiroho jirani kwani Dayosisi ya kusini magharibi mwa Tanganyika imekuwa na eneo kubwa hali inayofanya usimamizi wa maeneo hayo kuwa mgumu.

Naye mratibu wa mchakato wa uanzishwaji wa Dayosisi ya Mount Livingstone Kenani Andrew Hiluka alisema kimsingi vigezo vya kuanzishwa kwa Dayosisi mpya wilayani Ludewa yamekamilika na kutaja baadhi ya vigezo kuwa ni pamoja na uwepo wa wakristu wa kutosha, ukubwa wa eneo linalokusudiwa kuanzishwa.

Vigezo vingine ni kuwepo sanduku la posta/mawasiliano ya simu na miundombinu ya barabara, kuwepo na vyombo vya usafiri, kuwepo nw uwakili kuongezeka kwa waumini ilikukua kwa kanisa, kuwepo na wahudumu wa kutosha, kuwepo majengo ya ofisi na nyumba ya Askofu na fedha shilingi milioni 10 katika akaunti.

Tuna kila sababu ya kuanzisha Dayosisi nyingine kutokana na ukubwa wa eneo na wingi wa waamini hivyo kwa sasa tuko katika vikao vya mwanzo ili kukamilisha mchakato wa uanzishwaji wa dayosisi itakayotambulika kwa jina la Mount Livingstone na makao makuu ya Dayosisi hiyo yatakuwa Ludewa mjini”,alisema kenani Hiluka

Askofu Simalenga aliwataka viongozi na waamini wa dhehebu la Anglikana walioko wilaya ya Ludewa kuwa na mshikamano katika kufanikisha zoezi hilo kwani kuna taskforce ambayo imeundwa kushughurikia mchakato huo mpaka utakapo kamilika.

Doyasisi mpya ya mount livingstone yenye makao makuu yake mjini Ludewa inaundwa na mitaa/parokia 26 na kwa mujibu wa sensa ya mwaka 2011 Doyasisi mpya ina jumla ya waumini 32,800.

mwisho

No comments: