Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

July 27, 2013

CHAMA CHA WALIMU WILAYANI LUDEWA CHAPATA VIONGOZI WAPYA.




Katibu wa CWT mkoa wa Njombe Bi Luya Ngonyani akisoma matokeo ya uchaguzi katika ukumbi wa Halmashauri ya wilaya ya Ludewa
Mwenyekiti na muhasibu wa CWT wilaya ya Ludewa wakiwa na nyuso za furaha baada ya kushinda uchaguzi
Mhasibu mpya wa CWT wilaya ya Ludewa mwalimu Frolian Mtweve Mvanginye akiwa na furaha baada ya kushinda uchaguzi
Mwenyekiti mteule wa CWT wilaya ya Ludewa mwalimu Dominicus Mganwa baada ya kushinda uchaguzi
wajumbe wa chama cha walimu wilaya ya Ludewa wakiwa katika uchaguzi





Chama cha walimu (CWT)wilayani Ludewa katika mkoa wa Njombe hatimaye kimefanikiwa kuwapata viongozi wapya kupitia uchaguzi uliofanyika jana katika ukumbi wa Halmashauri ya wilaya hiyo kutokana na viongozi wa awali kustaafu na mwingine kupandishwa daraja.

Katika uchaguzi huo wanachama mbalimbali wa chama hicho waliweza kugombea uongozi katika ngazi ya mtunza hazina na mwenyekiti wa wilaya kwa kunadi sera zao kwa wajumbe waliohudhuria mkutano ili waweze kuziba nafasi hizo mbili na kupata washindi.

Akisoma matokeo ya uchaguzi huo katibu wa CWT mkoa wa Njombe Bi.Luya Ngonyani alizitaja sababu za kufanyika kwa uchaguzi huo ni kutokana na aliyekuwa mhasibu wa chama hicho Ignas Mkechi kustaafu katika utumishi wa umma na aliyekuwa mwenyekiti mwalimu Wiliam Kunyanja kuchaguliwa kuwa mjumbe wa kamati kuu ya CWT kupitia mkoa wa Njombe.

Bi.Ngonyani alisema kutokana na nafasi hizo kuwa wazi kwa muda mrefu na kufuatana na katiba ya chama cha walimu Tanzania imelazimu kuchagua viongozi wengine kupitia mkutano mkuu wa wilaya wa chama hicho ili kuziba nafasi hizo.

Katiba yetu inaruhusu kufanya uchaguzi kutokana na nafasi hizi zilizoachwa wazi hivyo kila mmoja ambaye ni mwanachama wa CWT anahaki ya kugombe na kuwa kiongozi katika chama chake lakini kwa kuwapata viongozi hawa ninahaika mmewachagua viongozi waadilifu na watendaji kazi wazuri na si vinginevyo”,alisema Bi.Ngonyani.

Katika uchaguzi huo ngazi ya uenyekiti wagombea walikuwa wane na matokeo yalikuwa kama ifuatavyo wapiga kura walikuwa 129 kura moja ilifaribika,Nzangwa Silingo alipata kura 3,Paulo ndimbo alipata kura 5,Ramon Lugome alipata kura 54 na Dominicus Mganwa alipata kura 65 hivyo kumfanya Dominicus Mganwa kuibuka kidedea na kuwa mwenyekiti wa CWT wilaya ya Ludewa.

Kwa ngazi ya Uhasibu kura zilizopigwa zilikua 129 ambapo Paulo ndimbo hakupata kitu,Elizabeth Suka alipata kura 3,George Martin 3,Amina haule 6,Mathayo Tematema kura 10,Aloysi Kapelela alipata kura 39 na Frolian Mtweve Mvanginye alipata kura 68 kwa matokeo hayo yalimfanya mwalimu Frolian Mtweve Mvanginye kuibuka kidedea na kupata nafasi ya Uhasibu wa CWT Ludewa.

Aidha Mhasibu mteule wa CWT wilaya ya Ludewa mara baada ya kuchaguliwa akiwashuguru wa Jumbe Mwalimu Frolian Mtweve Mvanginye alisema cheo hicho ni dhamana hivyo bila ushirikiano wa wajumbe hao hakuna ufanisi wowote wa kazi utakao undelea.

Bw.Mvanginye aliwataka wajumbe kutoa ushirikiano wa hali ya juu ili kuweza kutetea maslahi yao kwa mwajiri kwani umoja ni nguvu na utengano ni dhaifu hivyo kwa umoja wa walumu wote Tanzania hakuna kitakacho shindikana.

Nae Mwenyekiti mteule mwalimu Dominicus Mganwa aliwashukuru wajumbe kwa kumchagua na kutaka ushirikano daima baina ya wajumbe ili kubuni miradi mbalimbali itakyoweza kukiendesha chama hicho tofauti na michango wanayokatwa walimu hao kila wakati.

Mwalimu Mganwa alisema ifike wakati chama cha walimu Tanzania licha ya kupigania haki za wanachama kwa waajiri wao lakini kila wilaya kuwe na miradi endelevu itakayo wanufaisha wanachama katika kupata mikopo mbalimbali yenye riba nafuu.

Mwisho.


No comments: