Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

June 28, 2013

SHULE ZAKABILIWA NA UHABA WA MAJI LUDEWA



SHULE msingi nyingi wilayani Ludewa katika mkoa wa Njombe zinakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ya ukosefu wa maji safi na salama kwa ajili ya matumizi ya wanafunzi.

Hata hivyo changamoto hiyo inadaiwa kusababishwa na ongezeko la idadi ya wanafunzi kwa shule za msingi nchini,takwimu za kitaifa zinaonesha kuwepo na ongezekeko la asilimia 40.31 la wanafunzi kwa kipindi cha mwaka 2002 hadi 2011.

Mwenyekiti wa kamati ya shule ya msingi Madunda Bw.Chrisantus Haule alisema kuwa licha ya shule hiyo ya zamani kumilikiwa na kanisa Katoliki lakini bado miundombinu ya maji haina,hali inayosababisha wanafunzi kwenda kuchota maji kwenye mifereji iliyo mbali na shule,ambayo hata hivyo si safi na salama kwa ajili ya kunywa.

Baada ya kupata elimu kupitia mradi wa maji,Afya na usafi wa mazingira unaoendeshwa na shirika la Daraja,uongozi wa shule kwa kushirikiana na uongozi wa kijiji wamelipa kipaumbele suala hilo kwa kuanza na mkakati wakuchemsha maji na kuyahifadhi katika majaba kwa ajili ya matumizi ya wanafunzi ili kuwanusuru na maambukizi ya homa za matumbo na kuhara.

Ofisa elimu vielelezo wilaya ya Ludewa Bi.Helena Halifa aliwasisitiza walimu,wazazi na wanafunzi kuthamini utamaduni wa kuchemsha maji ya kunywa majumbani na ,shuleni ili kuwaepusha watoto na magonjwa yatokanayo na kunywa maji machafu,pamoja na kuzingatia usafi wa kunawa mikono kila wanapotoka choooni,hatua ambayo alisema itasaidia kupunguza gharama za matibabu.

“Jamani hili suala halihitaji gharama na ni kwaajili ya watoto wenu wenyewe,sasa usipolea mtoto wako unadhani nani atakulelea?Tupunguze matumizi yasiyo ya lazima tuweke hili suala mbele”,alisema Bi.Halifa.

Pamoja na kuwa maji huwa ya msimu katika eneo hilo,wazazi pamoja na walimu wameamua kutafuta maji kwa gharama yoyote pasipo kuwahusisha watoto wao ambao wanatakiwa kuwa darasani saa zote za masomo.

“Sisi tutapangiana zamu kulingana na vitongoji vyetu na tutajua jinsi gani tutachota maji na kuyaleta shuleni,wakati tukisuburi mkakati wa muda mrefu wa kuyafikisha maji shuleni”,alisema Bw.Joseph Kayombo,mmoja wa wazazi katika eneo hilo.

Mwisho.

No comments: