Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

June 25, 2013

DC LUDEWA AWATAKA WANAWAKE KUWAKATAA WANAUME WASIOFANYIWA TOHARA.



      


WANAWAKE Wilayani Ludewa katika Mkoa wa Njombe wametakiwa  kugoma kwa kukataa kufanya mapenzi na wanaume wasiofanyiwa tohara kama njia mojawapo ya ushiriki wao katika kampeni ya kupambana na kasi ya maambukizi ya virusi vya ukimwi wilayani humo.

Akizungumza jana Mkuu wa wilaya ya Ludewa Juma Madaha alisema wanawake wakiungana pamoja na kuamua kuwakataa wanaume wanaokwepa tohara watakuwa wamesaidia kwa asilimia 60 kupunguza kasi ya maambukizi ya virusi vya ukimwi na ukimwi wenyewe.

Madaha akaongeza kuwa suala la ukimwi limekuwa likipigiwa kelele kila kukicha kwa njia mbalimbali ikiwemo warsha, semina, makongamano na katika nyumba za ibada lakini lakini kasi ya maambukizi ya virusi vya ukimwi ndiyo yanazidi kuongezeka kila siku pengine ni kutokana na baadhi ya wanawake kutokuwa makini katika tendo la kujamiiana.

“” ninyi wanawake kataeni kabisa kufanya mapenzi na wanaume hao na wala msiwaonee aibu akina baba wanaokwepa kufanyiwa tohara kwa kisingizio cha mila kwani mkifanya hivyo mtakuwa mmelisaidia Taifa kupunguza kasi iliyopo sasa. ‘’’’ akasisitiza Madaha

Madaha alifikia hatua hiyo kutokana na takwimu kuonesha kuwa wilaya yake ndiyo inayosadikika kuongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya watu wanaoishi na virusi vya ukimwi ikilinganishwa na wilaya zingine zinazounda mkoa wa Njombe ambazo ni Makete, Njombe na Wanging’ombe.

Alisema mila na desturi ni tunu muhimu katika kuhakikisha uhai na ustawi wa jamii zetu lakini kuna haja ya kuzichambua mila na desturi na kuziendeleza zilizo nzuri na kuzikomesha zilizo mbaya zenye sura ya ukandamizaji, unyanyasaji, vitendo vya ukeketaji, ndoa zisizo rasmi, ubaguzi wa kijinsia na kurithi wajane.

Aidha Madaha alizitaja desturi nzuri kuwa ni pamoja na kuhimiza umuhimu wa kutekeleza tohara kwa watoto wa kiume na wanaume kwa kufanya hivyo tutapunguza kasi ya maambukisi ya virusi vya ukimwi na ukimwi katika jamii.

Kila jamii na familia ihakikishe inawatahadharisha watoto juu ya namna bora ya kujenga mienendo mizuri katika kusisitiza tabia njema zinazoendana na maadili na utamaduni wa mtanzania na kuepusha watoto juu ya kasumba ya kuiga mienendo ya michafu ya kimagharibi isiyo na tija kwa Taifa letu.

Mathalani mavazi na mitindo ya uvaaji usio na staha wala adabu, tabia na mienendo tete isiyoleta mantiki katika akili na zenye kupingana na maadili pamoja na mafundisho ya dini zetu kama vile ngono, mapenzi na ndoa za jinsia moja.

Na Bazil Makungu,Ludewa.


No comments: