Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

June 25, 2013

DAWA YA WATOTO WASIOJUA KUSOMA, IMEPATIKANA LUDEWA



ONGEZEKO la wanafunzi wasiojua kusoma, kuandika na kuhesabu katika wilaya ya Ludewa linasababishwa na watoto kuanza elimu wakiwa na umri mkubwa lakini pia linachangiwa na walimu kukaa muda mrefu bila kupata mafunzo mahali pa kazi.

Hayo yamebainishwa na shirika lisilokuwa la kiserikali la kitaliano la ACRA linalofanya miradi mbalimbali ya kijamii wilaya Ludewa katika Mkoa wa Njombe katika utafiti wake juu ya nini chanzo cha ongezeko la watoto wanaohitimu elimu ya msingi huku wakiwa hawajui kusoma, kuandika wala kuhesabu.

 Akizungumza katika warsha ya siku moja kwa maafisa elimu sekondari na msingi, walimu na wadau mbalimbali wa elimu meneja wa shirika hilo Beppe Buscaglia alisema madhumuni ya warsha ni kukutana na wadau wa elimu na kujadili kwa pamoja juu ya  mustakabali wa elimu  na changamoto zake wilayani Ludewa.

Beppe alisema shirika lake limefanya mambo mengi wilayani Ludewa ikiwa ni pamoja na ujenzi na ukarabati wa madarasa na nyumba za walimu kutokana na shule nyingine kuwa na vyumba vya madarasa ambavyo ama ni vibovu au vimechakaa.

Buscaglia akaongeza kuwa matokeo na mafanikio ya shirika la acra kuwagharimia mafunzo walimu kupitia chuo cha uwalimu cha Kreruu cha mjini Iringa kumeleta ufanisi mkubwa kwa walimu hao ikiwa ni pamoja na ongezeko la ufaulu na mahudhurio mazuri kwa wanafunzi.

Shirika hilo linalofanyakazi wilayani Ludewa limegundua kuwa watoto wengi wa kitanzania wanashindwa kumudu masomo kutokana na kukosa msingi wa elimu wakiwa wadogo na baadaye kurundikiwa mzigo mkubwa wa masomo wanapoanza darasa la kwanza na kuchanganyikiwa na kasha kuamua kuacha shule.

Ni kutokana na kuporomoka kwa elimu nchini, shirika lisilo kuwa la kiserikali la ACRA limeamua kuwapeleka mafunzo ya muda mfupi walimu wa shule za awali wasio na ajira serikalini na walimu wa shule za msingi wenye ajira kutoka kata za Mawengi, Milo na Mlangali wilayani Ludewa katika Mkoa wa Njombe ili waweze kufanyakazi zao kwa ufanisi.

Shirika hilo linalofanyakazi wilayani Ludewa limegundua kuwa watoto wengi wa kitanzania wanashindwa kumudu masomo kutokana na kukosa msingi wa elimu wakiwa wadogo na baadaye kurundikiwa mzigo mkubwa wa masomo wanapoanza darasa la kwanza na kuchanganyikiwa na kasha kuamua kuacha shule.

Hadi sasa shirika la ACRA limeshawapeleka mafunzo walimu 65 katika chuo cha ualimu cha Kreluu ambapo kati yao walimu 52 wanatoka katika shule za msingi na walimu 13 wanatoka katika shule za awali ambao hawana ajira serikalini.

Sababu zingine zilizotajwa na ACRA kama tatizo katika mfumo wa elimu ni pamoja na  walimu kukaa muda mrefu kazini bila kupata mafunzo ya mara kwa mara ili kwenda na wakati na walimu wa msingi kupewa kufundisha madarasa ya awali bila kuwa na mafunzo katika ngazi hiyo.

Naye Robert Hyera afisa elimu msingi wilaya ya Ludewa aliyealikwa kama mgeni rasmi, akifungua warsha hiyo alikiri kuwepo kwa wimbi la walimu waliokaa zaidi ya miaka kumi  tangu kuhitimu vyuoni ambao hadi sasa hawajawahi kupata mafunzo wala semina yoyote jambo ambalo linatishia kudidimiza elimu kwa sababu walimu hawaendi na wakati.

 “”” walimu wanahitaji kupata mafunzo ya mara kwa mara ili kwenda na wakati tena sambamba na mitaala lakini pamoja na kuyakabili mabadiliko yanayokea kila siku katikasekta ya elimu nchini.’’’’’ Alishauri Hyera

Aidha Bw Hyera alilisifu na kulipongeza shirika la acra kwa kugundua mapungufu hayo ambayo kimsingi kutokumwendeleza mwalimu ni kumdidimiza mwanafunzi kielimu na kwamba kama serikali itaiga mfumo huo basi itakuwa imeondoa na kufuta kabisa kuwepo kwa watoto wasiojua kusoma, kuandika na kuhesabu. 

“’’’’ tumekuwa na matatizo katika idara ya elimu kutokana na bajeti finyu ambayo imepelekea kudorora kwa elimu kwani walimu walio wengi hawapati mafunzo ya mara kwa mara ili kuboresha ujuzi na taaluma zao jambo ambalo linasababisha matokeo mabovu kwa wanafunzi”,akaongeza Bw.Hyera.

Katika mradi huo walimu wawili wa madarasa ya awali kutoa Ulayasi na Mlangali ambao wanajitolewa pasipo kuajiriwa serikalini walipata mafunzo ya miezi mitatu katika chuo cha ualimu Kreluu walipata mafunzo ya miezi mitatu na kuona mabadiliko makubwa.

Kwa upande wao walimu Tulamvona Mturo wa shule ya msingi mlangali na  Imelda Cassian Mtweve mwalimu wa shule ya awali ulayasi ambaye analipwa na jamii alisema mafunzohayo yamemsaidia na kumwongezea maarifa sana.

‘’’’’ kabla ya kupata mafunzo alikuwa akiingia darasani na kuanza kufundisha moja kwa moja bila ya kuwapa wanafunzi muda wa kucheza. Lakini kupitia mafunzo niliyoyapata nimeweza kuelewa saikolojia ya watoto na imekuwa rahisi kulimudu darasa kutokana na kuzitambua tabia tofauti za wanafunzi anaowafundisha.

 “Natumia zana za kufundishia na kujifunzia pia nafurahia ufundishaji wangu wa sasa kuliko zamani kwani awali sikujua jinsi ya kumudu na kupanga ufundishaji wangu,nilitumia jitihada nyingi kufundisha lakini wanaojiunga darasa la kwanza takribani nusu yao walikuwa hawajui kusoma

MWISHO.

No comments: