Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

May 05, 2013

WANANCHI WA KIJIJI CHA MBWILA KATA YA LUANA WILAYANI LUDEWA WAMLALAMIKIA MKANDARASI KWA KUCHELEWESHA MRADI WA MAJI



Chanzo cha maji hayo ambapo pametegwa(intake) pakiwa pamebomoka baada ya kujengwa kabla ya kuisha ujenzi wa mradi huo.
Mwananchi akiwaonesha waandishi wa habari jinsi uchanganyaji wa saruji na mchanga ulikoa chini ya kiwango ndio sababu kubwa ya kubomoka kwa bwawa hilo.
Ukuta wa bwawa la kukusanyia maji ukiwa umebomoka
kulia ni mwandishi wa mtandao huu Bw.Nickson Mahundi akiwa na wananchi eneo la ujenzi wa bwawa la kukusanyia maji kijiji Mbwila
Ukubw wa bomba lililotegwa katika chanzo hicho haukidhi viwango vya usambazaji maji kutoka intake kwenda kwa wananchi wa kijiji cha Mbwila ukilinganisha na uwingi wa wanakijiji wa kijiji hicho.
 wananchi wakiangalia ujenzi wa intake hiyo ulioanza kubomoka
haya ndio maji katika mradi huo
Mwandishi wa mtandao huu akiangalia bomba zilikoelekea
 Safari ya kuelekea katika safu ya milima livingstone ambako intake hiyo imejengwa
Waandishi wa habari wakitembea kwa miguu kuifuata intake hiyo
 Hili ndilo bomba kuu linalotoka katika intake hiyo na kwenda kwa wananchi,ni mradi uliogharimu shilingi 243 milioni lakini bado haujakamilika kwa kusuasua kwa wakandarasi
Bomba kuu la kutoa maji intake
safari ya intake ikiwa inaendelea
Bomba kuu kutoka intake
Wanahabari wakikaribia intake


Bomba kuu la kutoka intake
misitu iliyoko safu za milima livingstone
ukuta ukiwa umebomoka
intake ikiwa imebomoka
bwawa la kukusanyia maji likiwa limejengwa lakini badop maji yanapita chini ya intake hiyo
 maji yakiingia katika bwawa hilo
                     bomba kuu linalotoka intake

Wananchi wa kijiji cha Mbwila wilayani Ludewa katika mkoa wa Njombe wamemlalamikia mkandarasi wa kampuni ya Northern Costruction ltd kwa kusuasua katika ujenzi wa mradi wa maji ambao ni ukombozi kwa kijiji hicho.

Akitoa malalamiko hayo mbele ya waandishi wa habari waliotembelea mradi huo mmoja wa wananchi wa kijiji cha Mbwila Bi.Mariam Haule alisema kijiji hicho kimekuwa na tatizo la upatikanaji wa maji safi na salama kwa muda mrefu lakini chakushangaza Serikali imetoa fedha ili kutatua tatizo hilo na aliyekabidhiwa fedha hizo anasuasua kujenga mradi huo.

Bi.Mariam alisema tatizo la maji wanaopata tabu zaidi ni wanawake kutokana na umbali mrefu wanaotembea kufuata maji hayo,wao kama wananchi walifurahia sana kitendo cha Serikali kutopa fedha hizo lakini hata eneo la kutega maji hayo limejengwa chini ya kiwango.

Mwenyekiti wa kijiji hicho Bw.Gerod Haule alisema ujenzi wa chanzo cha maji hayo ulikuwa ukiendelea vizuri lakini mpaka sasa ni zaidi ya miezi miwili kampuni hiyo haionekani kijijini hapo bila ya taarifa yoyote ikiwa hata ujenzi wa awali umeanza kubomoka.

Bw.Haule alimtaja msimamizi wa mradi huo ambao umegharimu shilingi 243 milioni kuwa ni George Mpilima ambaye amekuwa akiahidi kuukamilisha mradi huo ndani ya mienzi sita lakini kwa mujibu wa mkataba wa mradi huo ni mwaka mmoja ambapo mpaka sasa umebaki mwezi mmoja na nusu na hakuna kinachoendelea.

“Tumeshangazwa na mwenendo wa ujenzi wa mradi huu kutokana na hata ujenzi wa eneo ambako maji hayo yatatengwa uko chini ya kiwango na umeshaanza kubomoka kabla mradi haujakamilika sasa bado hatuelewi ni kitu gani kinaendelea ili mradi huu ukamilike”,alisema Bw.Haule.

Msimamizi wa mradi huo Mhandisi George Mpilima alikili kuwa yeye ndiye msimamizi na akamtaja mkurugenzi wa Kampuni ya Northern Contruction ltd ndiye aliyeshika ukandarasi na kumuajiri yeye lakini kutokana na sababu zisizozuilika mradi huo umekuwa ukisuasua lakini utakamilika.

Bw.Mpilima alijitetea kwa kusema muda wa kukabidhi mradi huo bado haujafikia hivyo kwa muda mwa mwezi mmoja na nusu mradi huo utakamilika na kuwataka wananchi wasiwe na wasiwasi na kampuni yake kwani inauzoefu na kazi za namna hiyo.

Aidha Muhandisi wa maji katika Halmashauri ya wilaya ya Ludewa Bw.Athanasius Munge alisema mradi huo ulioanza Julai 2012 unatarajia kumalizika Julai mwaka huu lakini mpaka sasa hauko katika hali nzuri kutokana na mkandarasi huyo kuondoka bila taarifa katika eneo la mradi kwa zaidi ya miezi miwili.

Bw.Munge alisema mkandarasi huyo amekuwa msumbufu kwa kutopatikana kwa muda mrefu hata akipigiwa simu yake ya mkononi wakati mwingine kushindwa kupokea kutokana na kutokuwa na sababu za msingi za kusiotisha mradi huo.

“Tumekuwa tukimtafuta na taarifa kwa maandishi nimeziwasilisha kwa mkurugenzi wa halmashauri ambapo alimuandikia barua ya onyo Februali mwaka huu  bado ni mkaidi tuansikia amekuja huko hapa wilayani lakini tunajaribu kuangalia namna ya kufanya katika mkataba wake”,alisema Bw.Munge.

Bw.Munge alisema hata ujenzi wa chanzo cha maji hayo(intake)unaonekana uko chini ya kiwango kutokana bado mradi huo haujaisha ni mwenzi mmoja umebaki lakini umeshaanza kubomoka baadhi ya kuta.

Mkurugenzi wa kampuni ya Northern construction ltd ambayo inajenga mradi huo aliyejitambulisha kwa jina moja la Mchenya alipotakiwa kuutolea maelezo kwa njia ya simu ya kiganjani alijibu yeye si msemaji  wa mradi.

Mwisho.

No comments: