Wananchi
wa kijiji cha Ilele kata ya Ruhuhu wilayani Ludewa katika mkoa wa
Njombe wamewasimamisha kazi mwenyekiti wa kijiji hicho pamoja na
mtendaji kwa kile kinachodaiwa kushindwa kusimamia maendeleo.
Akizungumza
na waandishi wa Afisa mtendaji wa kata ya Ruhuhu Bw.Ashery Lufingo
alisema maamuzi hayo ya wananchi yamefikia kutokana na viongozi hao
wawili kushindwa kusimamia shughuri za maendeleo katika kijiji hicho.
Bw.Lufingo
alisema Mey 5 mwaka huu katika mkutano wa hadhara ulioitishwa na
viongozi hao kwa lengo la kusoma mapato na matumizi ya kijiji hicho
na baada ya kusoma taarifa ya kijiji wananchi hao waliipinga vikali
taarifa hiyo na kuwatimua.
Akiwataja
viongozi hao waliofukuzwa kazi na wananchi Bw.Lufingo alisema
mwenyekiti wa kijiji anafahamika kwa jina la John Tendeka na mtendaji
wa kijiji hicho anatambulika kwa jina la Esau Haule.
“Tumepokea
malalamiko kutoka kwa wananchi lakini wao ndio wenye uamuzi na
mwenyekiti wao na kuhusiana na mtendaji nimeshapeleka taarifa katika
ngazi husika na tuko katika kuchagua viongozi wa muda ili kijiji
kiweze kuendelea na majukumu yake”,alisema Bw.Lufingo.
Alisema
wananchi hao wamekasilishwa baada ya kuona baina ya viongozi hao kati
ya mwenyekiti na mtendaji hawapatani na ndio sababu kuu ya kijiji
hicho kufifia kimaendeleo kwa muda mrefu na hakuna suruhu ya viongozi
hao wawili inayopatikana.
Aidha
Diwani wa kata ya Ruhuhu Bw.Edwin Haule Spika alifafanua kuwa sababu
ya viongozi hao kukataliwa na wananchi ni kushindwa kusimamia
shughuri za maendeleo zikiwemo ufyatuaji wa tofari za ujenzi wa
zahanati.
Bw.Spika
alisema wananchi walijitolea nguvu zao katika ufyatuaji wa tofari
hizo lakini chakushangaza zimeshindwa kuhifadhiwa vizuri na kufikia
baadhi ya tofari kuharibiwa vibaya na mvua.
Alisema
taarifa zimeshafika katika ngazi husika hivyo kinachofuata ni
uchaguzi wa viongozi wa muda ili kijiji hicho kiweze kufanya kazi za
maendeleo kama awali.
Aidha
aliyekuwa mtendaji wa kijiji hicho Bw.Esau Haule alipohojiwa na
waandishi wa habari alikili kuwepo kwa tukio la wao kukataliwa na
wananchi lakini aliwalaumu wananchi kwa kushindwa kutekeleza kazi
walizo kubaliana.
Bw.Haule
alisema moja ya kazi walizokubaliana ni ukataji wa nyasi na kuyaezeka
matanuli ya matofari hayo ili yasiharibiwe na mvua lakini wananchi
hao walikaidi agizo hilo na kuikataa taarifa ya mapato na matumizi ya
kijiji.
Alisema
wao wameyapokea maamuzi hayo ya wananchi kwa mshtuko kwani
hawakutegemea kutokana na utendaji wao wa kazi licha ya kutoa maagizo
kwa wananchi ili kuleta ufanisi wa kijiji hicho katika maendeleo na
kupingwa vikali.
Mwisho
No comments:
Post a Comment