Mkuu wa mkoa
wa Njombe kapteni mstaafu Assery Msangi jana aliwatembelea wachimbaji wadogo wa
madini wilayani Ludewa ikiwa ni moja ya ziara yake ya kutambua aina ya madini
yanayopatikana wilayani humo.
Katika ziara
hiyo Kepteni Msangi aliweza kutembelea machimbo ya dhahabu na shaba katika kata
ya Nkomang’ombe eneo la Muhumbi ambako aliweza kuongea na wananchi pamoja na
wachimbaji wadogo ambao waliweza kutoa kero mbalimbali zinazowakabili na baadae
kwenda machimbo ya dhahabu yaliyoko kijiji cha amani kata ya Mundindi.
Akiongea na
wananchi pamoja na wachimbaji wadogo Kamteni Msangi aliwasisitiza wananchi hao
umuhimu wa kuwapeleka watoto wao shule ili waje kuwa warithi wazuri wa machimbo
hayo.
“ni vema
watoto wenu wakapata elimu ili waje kunufaika na migodi hii kuliko kuishi nao
polini bila ya kuwapeleka shule lakini katika migodi ndiko maambukizi ya ukimwi
yanakoshamili hivyo mnatakiwa kuwa waangalifu katika kazi zenu”,alisema Kapteni
Msangi.
Kapten
Msangi alisema mkoa wa Njombe unaongoza katika maambukizi ya virusi vya Ukimwi
nchini hivyo kila mchimbaji anatakiwa kuwa mwangalifu kwani sio sifa nzuri
kuongoza kwa jambo hilo bali kushirikiana kujitoa katika sifa hiyo mbaya.
Wilaya ya
Ludewa inazaidi ya aina saba za madini ambapo kuna maeneo wamepewa wawekezaji
wan je na maeneo mengine yamekaliwa na wawekezaji wa ndani ambao bado
hawajaanza uchimbaji na kuyaacha maeneo hayo yakiwa misitu mikubwa.
Akitoa kero
zinazowakabili wachimbaji wadogo John Hiluka alisema kumekuwa na mkanganyiko wa
mipaka katika kata Nkomang’ombe kati ya wachimbaji wakubwa na wadogo hali
ambayo inawanyima uhuru wachimbaji wadogo.
Bw.Hiluka
alisema awali wanchi wa kitongoji cha Muhumbi walikubaliana na shirika la
Maendeleo la Taifa(NDC)mwisho wa maeneo ya wawekezaji lakini cha kushangaza
wawekezaji hao wamevuka mipaka na kuingia katika eneo wanaloishi wananchi.
Alisema eneo
ambalo walipewa wawekezaji wa kampuni ya M.M.I lilikuwa ni lile lenye makaa yam
awe lakini baada ya kuona eneo wanaloishi wananchi lina madini aina nyingine
yakiwemo ya shaba na dhahabu ndiko waliko wachimbaji wadogo kampuni hiyo
imevuka na kufika huko.
Bw.Hiluka
alisema ni vema Serikali kupitia shirika la maendeleo la taifa(NDC) wakatenga
mapema eneo la wachimbaji wadogo ili waweze kujipatia rizki kwani bila ya
kufanya hivyo wachimbaji hao na wawekezaji wanaweza kusababisha madhara
makubwa.
Nae
msimamizi wa wacimbaji wadogo katika machimbo ya dhahabu Amani Bw.Samwel
Kabelege alimwomba mkuu wa mkoa kuangalia upya mipaka ya eneo la wachimbaji
wadogo katika eneo lao kutokana na eneo hilo kuwa finyu.
Bw.Kabelege
alisema inasikitisha kila wanapotaka kupanua eneo la uchimbaji wanaambiwa na
mamlaka kuwa maeneo yote yanawatu hali ambayo inayowafanya wachimbaji wadogo kurudia
maeneo hay ohayo katika uchimbaji.
“inasikitisha
kuona kila tukienda ofisi ya madini ya kanda mkoani Mbeya majibu tunayopata ni
kwamba maeneo yote ya wilaya ya Ludewa yanawatu tayari wakati hayafanyiwi
kazi,tunachokiomba kwa Serikali itutengee maeneo sisi wazawa wachimbaji wadogo
badala ya kuyauza maeneo yote katika nchi yetu”,alisema Bw.Kabelege.
Aidha Mkuu
wa wilaya ya Ludewa Bw.Juma Solomon Madaha aliwataka wachimbaji hao kuwa
watulizu na kuyatoa malalamiko yao kwa maandishi ili yaweze kufanyiwa kazi
kwani hakuna jambo lisiloweza kutatulika.
Bw.Madaha
aliwahimiza wachimbaji hao kulipa kodi ili halmashauri iweze kupata mapato
kwani kunawachimbaji wadogo wengi ambao wamejiunga katika vikundi mbalimbali
lakini hawataki kulipa kodi licha ya kuwa wanazitumia barabra za halmashauri
hiyo kusafirisha shaba.
Alisema
wachimbaji wamekuwa wakikwepa kodi kwa kusingizia wanailipa wizara hali ambayo
inainyima mapato Halmashauri,kwa kuangalia hilo hata ruhusiwa mchimbaji yeyote
kupitisha madini yake bila kulipia ushuru.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment