Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

April 27, 2013

SHIRIKA LA ACRA LAKUTANA NA WADAU WA ELIMU WILAYANI LUDEWA.



 
Shirika sililo la kiserikali la kiitaliano la ACRA linalofanya kazi wilayani Ludewa katika mkoa wa Njombe jana limekutana na wadau mbalimbali wa elimu wilayani huo ili kujua muhustakabali wa elimu na changamoto zake.

Warsha hiyo iliyofanywa katika ukumbi wa Halmashauri ya wilaya ya Ludewa iliwashirikisha pia walimu waliowezeshwa na shirika hilo katika mafunzo mbalimbali ya elimu ya msingi katika madarasa ya awali ilikujenga misingi bora ya elimu kuanzia ngazi ya chini.

Akifungua warsha hiyo ambayo ilikwenda sambamba na wiki ya elimu Duniani ambayo huazimishwa kila mwaka Aprili 21 hadi 28 kwa mwaka 2013 ilikiwa na kauli mbiu ya kila mtoto anahitaji mwalimu Afisa elimu wa wilaya ya Ludewa Robart Hyera alisema walimu wanahitaji mafunzo ya mara kwa mara.

Bw.Hyera alilisifu shirika la acra kwa kufanya mambo mengi katika elimu kwa wilaya ya Ludewa yakiwemo ya ujenzi wa vyumba vya madarasa katika kata za Mlangali,Mawengi na Milo pia kutoa mafunzo kwa walimu wa madarasa ya awali.

Alisema kumekuwa na wimbi la walimu ambao tokea walipohitimu vyuoni hawajawahi kupata mafunzo tena zaidi ya miaka kumi hali ambayo inazoofisha elimu za Tanzania na ndicho chanzo kikuu cha kuzorota kwa elimu.

“Tumekuwa na matatizo katika idara ya elimu kutokana na bajeti finyu ambayo imepelekea kudorora kwa elimu kwani walimu walio wengi hawapati mafunzo ya mara kwa mara ili kuboresha ujuzi wao jambo ambalo linasababisha matokeo mabovu kwa wanafunzi”,alisema Bw.Hyera.

Meneja mradi wa ACRA Bw.Beppe Buscaglia alisema shirika lake limefanya mambo mengi wilayani Ludewa hasa katika ujenzi wa madarasa na nyumba za walimu kutokana na shule nyingine kuwa na vyumba vya madarasa vibovu.

Bw.Buscaglia alisema matokeo ya shirika la acra kutoa mafunzo kwa walimu kupitia chuo cha uwalimu cha Kreruu kumeleta ufanisi mkubwa ikiwa pamoja na ongezeko la ufaulu na mahudhurio yawanafunzi.

Alisema mpaka sasa jumla ya walimu wawili walipata mafunzo ambao ni mwalimu Tulamvona Mturo miaka 52 wa shule ya msingi Mlangali ambaye anafundisha darasa la pili na mwalimu Imelda Cassian Mtweve miaka 38 wa shule ya awali ulayasi ambaye analipwa na jamii.

Aidha mwalimu Imelda Mtweve anayefundisha madarasa ya awali katika shule ya msingi Ulayasi alisema kabla ya kupata mafunzo alikuwa akiingia darasani na kuanza kufundisha moja kwa moja bila ya kuwapa wanafunzi muda wa kucheza.

Alisema wanafunzi walikuwa wanachoka mapema kutokana kutokujua mpangilio wa ufundishaji hali ambayo ilipelekea wanafunzi karibia nusu ya darasa kutokujua kusoma na kuandika pindi waingiapo darasa la kwanza.

Mwalimu Imelda alisema kupitia mafunzo aliyoyapata kutoka shirika la acra ameweza kuelewa saikolojia ya watoto na imekuwa rahisi kilimudu darasa kutokana na kuzitambua tabia tofauti tofauti za wanafunzi anaowafundisha.

“Natumia zana za kufundishia na kujifunzia pia nafurahia ufundishaji wangu wa sasa kuliko zamani kwani awali sikujua jinsi ya kumudu na kupanga ufundishaji wangu,nilitumia jitihada nyingi kufundisha lakini wanaojiunga darasa la kwanza takribani nusu yao walikuwa hawajui kusoma na kuandika”,alisema mwalimu Imelda.

Nae Afisa maendeleo ya jamii wa shirika la ACRA Bi.Neema Lazaro alisema licha ya ujenzi na mafunzo yanayotolewa na shirika lake pia wanatoa viotabu vya masomo ya hisabati na kiingereza katika shule za msingi za kata ya Milo,Mlangali na Mawengi.

Bi.Neema alisema pia baadhi ya madarasa ya awali katika kata hizo wametoa vifaa vya kuchezea watoto na kuchora michoro katika kuta za madarasa hayo ambapo picha hizo husaidia watoto kutambua vitu mbalimbali.

Mwisho.

No comments: