Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

April 25, 2013

IVA YOUTH GROUP WAPANIA KUREKODI FILAMU YENYE MAZINGIRA HALISI YA WILAYA YA LUDEWA





Kikundi cha sanaa chenye makao yake makuu wilayani Ludewa katika mkoa wa Njombe kimepania kuandaa Filamu itakayoonesha uhalisia wa mazingira ya wilaya hiyo kutokana na vivutio vinavyopatikana ili kuitambulisha wilaya katika ulimwengu wa sanaa.

Hayo yalisemwa jana na katibu wa IVA YOUTH GROUP Bi.Elizabeth Haule ambaye ni mjumbe wa halmashauri kuu ya CCM (NEC) wakati wa mazoezi ya filamu hiyo katika ukumbi wa ccm wilaya ya Ludewa.

Bi.Elizabeth alisema kutokana na uhalisia na madhari nzuri ya wilaya ya Ludewa iliyopambwa na milima yenye uoto wa asili,ziwa nyasa,machimbo ya dhahabu na makaa yam awe bila kusahau chuma cha liganga filamu hiyo itakuwa ya kwanza kuonesha vivutio vya asili.

Alisema wilaya ya Ludewa ina wasanii wengi ambao bado hawajapata msukumo wa kuonesha vipaji vyao hivyo ni fulsa pekee kwa wasanii hao kuungana na kufanya sanaa itakayoitambulisha wilaya hiyo na vivutio vyake.

“Vijana wengi wanapenda kuonesha uwezo wao katika sanaa mbalimbali lakini bado hawajapata wadau wa kuwasaidia kuitangaza wilaya hii kwani inavivutio vingi ambavyo havipatikani katika maeneo mengine nchini”,alisema Bi.Elizabeth.

Kundi hilo limesajiriwa na Baraza la Sanaa la Taifa(BASATA) pia limeweza kufanya kazi za uelimishaji hasa katika masuala ya afya kupitia mashirika mbalimbali lakini bado halina mfadhiri ambaye ameweza kulisaidia kwa chochote zaidi ya wasanii wenyewe kujichangisha ili kuendeleza sanaa zao.

Afisa utamaduni wa wilaya ya Ludewa Bw.Shaban Bakari alisema yeye ndiye mwalimu pekee aliyejitolea kwa wakati huu kulifundisha katika sanaa mbalimbali kutokana na kutokuwa na mwalimu kwa kipindi kirefu.

Bw.Shaban alisema vijana wengi wameweza kujiunga mpaka sasa jumla ya vijana 26 wamekuwa wakihudhuria mazoezi ya Filamu hiyo na michezo mingine lakini bado wanakabiliwa na changamoto nyingi.

Alisema changamoto kubwa ya IVA YOUTH GROUP ni ukosefu wa vyombo vya sanaa kutokana na wilaya hiyo kutokuwa na mwamko mkubwa wa makundi ya sanaa kwani hilo ni kundi pekee ambalo limeweza kuonesha uhai.

Bw.Shabani alisema baada ya kukamilisha mazoezi ya awali kundi hilo litafanya uzinduzi rasmi wilayani humo ili kujitambulisha rasmi hivyo wadau mbalimbali wataalikwa ili kutoa maoni yao yatakayoweza kuwaendeleza vijana hao katika tasnia ya sanaa.

Aidha Suzan Ng’ingo ambaye ni kaimu mwenyekiti wa IVA YOUTH GROUP aliwataka wasanii wa kundi hilo kuwa wavumilivu kutokana na hali ngumu ya kifedha inayolikabili kundi hilo.

Bi.Suzan uhalisia wa filamu hiyo na mazingiora ya wilaya ya Ludewa ndio sifa pekee itakayoweza kuwapatia heshima wasanii wa kundi hilo hasa kutokana na ukweli kwamba hakuna kundi lolote la sanaa lililoweza rekodi filamu katika mazingira ya Ludewa.

Mwisho.

No comments: