Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

April 05, 2013

NJOCOBA YAPANUA HUDUMA ZA KIBENKI LUDEWA, MAKETE.



 Wadau mbalimbali katika ukimbi wa Halmashauri ya wilaya ya Ludewa wakifuatilia maelezo kutoka kwa mkurugenzi wa NJOCOBA
Mwandishi wa habari wa gazeti la mwananchi Bw.Bazil Makungu akihojiana na afisa mikopo wa bank ya NJICOBA Bw.Danford Mfikwa
Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Ludewa Bw.Wiliam Waziri katika warsha hiyo ndani ya ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Ludewa

wadau wakitoa maoni yao jinsi ya ufanyaji kazi wa bank ya wananchi Njombe(NJOCOBA)
Kulia ni Mkurugenzi wa bank ya NJOCOBA Bw.Michael Ngwira akiwa na afisa ushirika wa mkoa wa Njombe Bw.Thomas Nyamba wakiandika maoni ya wadau.


Bank ya wananchi Njombe(NJOCOBA)yenye makao yake mkuu mkoani Njombe imeamua kupanua huduma zake kwa kufungua vituo vyake katika wilaya za Ludewa,Makete na mji wa Makambako ili kuweza kuwafikishia huduma hiyo wateja wake.

Akizungumza jana wilayani Ludewa Mkurugenzi mtendaji wa Bank hiyo Michael Ngwira aliitaka Halmashauri ya wilaya ya Ludewa kutenga fedha kwa ajili ya kununua hisa katika benki hiyo ya wananchi na kuwahamasisha watumishi na wananchi kununua hisa ili kukidhi vigezo vya kufungua kituo cha kutolea huduma za kibenki.

Ngwira pamoja na wataalamu wengine walitembelea wateja wa banki ya Njokoba katika wilaya ya Ludewa wakiwa na lengo la kutoa ufafanuzi kuhusiana na masula ya mikopo na manufaa ya saccos katika kupitia benki hiyo.

“”” benki ya Njocoba ya mjini njombe ni mali ya wananchi wa wilaya zote za mkoa wa Njombe hivyo ni fulsa pekee kwa wananchi hao kunufaika nayo kwa kupata mikopo midogo midogo itakayowawezesha kufungua biashara za kuwasaidia kuondokana na umaskini.””” Alisema Ngwira

Naye afisa mikopo wa Njocoba Danford Mfikwa akawataka wateja wake kuwa na subira kwani vituo hivyo vinatarajia kuanza rasmi juni mwaka huu ili kwenda sambamba na changamoto zinazowakabili wananchi hasa wajasliamali wadogowadogo wasiokopesheka na makampuni mengine nao waweze kukopa na kujiendesha kimaisha.

Bw.Mfikwa alisema bank hiyo pia hutoa huduma za mikopo ya pembejeo kwa wateja wake pindi wanapohitaji mikopo hiyo hivyo ni fulsa pekee kwa wateja wakulima kuchangamkia mikopo hiyo.

Aliwataka wakulima wa wilaya ya Ludewa na makete kujiunga na saccos mbalimbali ili waweze kukopesheka kwani wakulima wa wilaya ya Njombe wameweza kunufaika na bank hiyo kupitia vikundi vya kuweka na kukopa.

Nao washiriki wa warsha hiyo wilayani Ludewa walifurahishwa na kuunga mkono jitihada za benki ya Njocoba na kwamba wamechoshwa na usumbufu wa kutumia benki moja na kuomba uongozi huo kufanya haraka kufungua tawi kwani wako tayari.

 Katika ziara hiyo mkurugenzi wa njocoba alifanikiwa kuzungumza na kikundi cha Rafiki ambacho kinataria kusajiriwa hivi karibuni na kuwa mwanachama wa Njocoba.

Aidha Bw.Ngwira aliwataka viongozi wa kikundi cha Rafiki kuutangazia umma ili wananchi wengi waweze kujiunga na kikundi hicho kitakachoweza kupata mikopo kutoka bank mbalimbali.

Mwisho.



No comments: