Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

March 14, 2013

WANANCHI WILAYANI LUDEWA WATAKIWA KUTOA USHIRIKIANO KWA MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI




Wananchi wa wilaya ya Ludewa katika mkoa wa Njombe wametakiwa kuyapa ushirikiano mashirika yasiyo ya kiserikali yanayokwenda kufanya kazi katika maeneo yao ili kuleta maendeleo kwani kumekuwa na ugumu mkubwa kwa mashirika hayo katika utekelezaji wa miradi vijijini.

Hayo yamesemwa jana na mratibu wa miradi ya ujenzi wa shirika la ACRA kupitia mradi wa INTERVITA Bi.Neema Kidugo wakati akikabidhi chumba cha darasa kilichojengwa na shirika hilo kwa kushirikiana na wananchi katika shule ya msingi Mawengi.

Bi.Neema alisema kumekuwa na ugumu mkubwa wa kazi katika baadhi ya vijiji wilayani Ludewa kwa mashirika yasiyo ya kiserikali eidha kwa viongozi wa vijiji ama kwa wananchi wenyewe hivyo wananchi wanapaswa kuelimishwa ili kushiriki kikamilifu katika miradi inayotekelezwa katika vijiji vyao ili kuleta maendeleo zaidi vijijini.

Shirika hilo la ACRA kupitia mradi wa  INTERVITA lenye makao yake makuu nchini Italia limekuwa likijishughurisha na miradi mbalimbali ya kijamii nchini ikiwemo miradi ya umeme vijijini,afya,maji,elimu na ujenzi wa vyumba vya madarasa na vyoo salama.

Akisoma taarifa ya ujenzi wa chumba hicho cha darasa Bi.Neema alisema ujenzi huo wa darasa la shule ya msingi Mawengi umegharimu jumla ya shilingi million 19 na laki 5 kati ya fedha hizo shilingi million 16 zilitolewa na shirika la ACRA kupitia mradi wa INTERVITA na shilingi million 3.5 ni nguvu za wananchi wenyewe.

“Jengo hilo tulitakiwa tuwakabidhi Januari mwaka huu lakini kutokana na wananchi kuwa nyumba katika shughuri mbalimbali za kimaendeleo tumeshindwa kulikabidhi kwa wakati lakini bado tunaujenzi wa jengo jingine la darasa la awali hivyo tunaomba wananchi watupatie ushirikiano wa kutosha sio sisi tu hata mashirika mengine ili kukamilisha haraka miradi iaanyotekelezwa”,alisema Bi.Neema.

Bi.Neema alisema ACRA wanakusudia kuendeleza ukarabati na ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule tano ambapo ujenzi huo utafanyika katika kata ya Mawengi,Milo na Mlangali hivyo wananchi wa kata hizo wanatakiwa kijiandaa katika utekelezaji wa miradi ya ujenzi kwa wakati.

Akikabidhiwa jengo hilo la darasa Afisa elimu wa wilaya ya Ludewa Bw.Robart Hyera  alilishukuru shirika la ACRA kupitia mradia wa INTERVITA kutoka na shirika hilo kutekeleza miradi mingi na mikubwa katika wilaya ya ludewa inayowanufaisha wananchi moja kwa moja.

Bw.Hyera alisema ifike wakati wananchi waoneshe mchango wao kwa wafadhiri kama hao kwani wamekuwa waiiunga mkono Serikali katika kufikisha maendeleo vijijini hivyo hakuna sababu ya viongozi wa vijiji na wananchi kukwamisha miradi ya maendeleo isitekelezwe.

Alisema kumekuwa na changamoto nyingi katika shule za msingi wilayani Ludewa ikiwemo uhaba wa vyumba vya madarasa lakini kupitia mashirika mbalimbali likiwemo shirika la ACRA ukarabati na ujenzi wa madarasa umekuwa ukifanyika hivyo Serikali haina budi kuyapongeza mashirika ya namna hiyo kutokana na juhudi yanayozifanya katika kuboresha madarasa nchini.

Bw.Hyera aliyataka mashirika mengine kuiga mfano wa shirika la ACRA katika kuhudumia wananchi vijijini badala ya kujikita mjini ambako hakuna changamoto kubwa za kimaisha kwani wananchi wa vijijini wakielimishwa wanaweza kutoa ushirikiano katika utekelezaji wa miradi mbalimbali.

Aidha meneja mradi wa shirika la ACRA Bw.Beppe Buscaglia shirika hilo lilianza kufanya kazi nchini mwaka 2006 katika jimbo katoriki la Njombe likitekeleza miradi ya umeme na kuendeleza miradi ya ujenzi kupitia shirika la SHIPO kama mkandarasi katika miradi ya ujenzi.

Shirika hilo la ACRA limeanza kusambaza nishati ya umeme katika shule kumi ikiwa ni kata ya Milo shule tano na kata ya Mawengi shule tano ili kuwawezesha wanafunzi wa shule hizo kuweza kujisomea masomo ya jioni bila matatizo.

Naye fundi mkuu msanifu wa shirika la SHIPO Bw.Vicent Mgina ambaye pia ni diwani wa kata ya Mundindi alisema kupitia ACRA wamekuwa wakijenga na kutoa mafunzo kwa mafundi ujenzi wa vijijini ili kuwawezeshz mafundi hao kwenda na wakati.

Bw.Mgina alisema mafundi walioshiriki katika ujenzi wa jango la darasa la shule ya msingi Mawengi wametunukiwa vyeti kutokana na kazi nzuri waliyoifanya hivyo aliwasihi mafundi wa vijiji vingine ambako ujenzi utaendelea kujitokea ili kunufaika na mafunzo yatakayotolewa na SHIPO.

 Mwisho.


No comments: