Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

March 05, 2013

MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA LUDEWA ASHINDA KESHI YA RUSHWA.




         
Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Ludewa Bw.Matei Felisian Kongo jana alisinda kesi iliyokuwa ikimkabili ya kuomba na kupokea rushwa kwa Bw.Solomon Mwaikugile machi 14,mwaka 2012 na kuachiwa huru katika mahaka ya wilaya ya Ludewa.

Akisoma hukumu hiyo katika mahaka ya wilaya Hakimu mkazi mfawidhi wa wilaya ya Ludewa Mh.Frederik Lukuna alisema sababu ya kwanza iliyomfanya mshtakiwa aachiwe huru ilikuwa upande wa mashtaka ulishindwa kuthibitisha kwa maandishi kuwa Bw.Matei Kongo alikuwa anakesi ya kujibu.

Mh.Lukuna alisema sababu ya pili ilikuwa shahidi namba moja ambaye ni Bw.Solomon Mwaikugile alimtafuta Bw.Kongo ili amshawishi na si kongo aliyemshawishi Bw.Mwaikugile.

Sababu ya tatu ilikuwa ni kampuni ya Bw.Mwaikugile haikuomba tenda na hakuna sehemu inayoonesha Bw.Kongo aliomba rushwa ya shilingi million tatu,pia alipewa fedha ya mafuta kupitia katika account ya Aidan Luoga katika bank ya NMB tawi la Ludewa na kabla hajapata fedha hiyo tayari mwenye  ambako fedha ilipitia akakamatwa.

Bw.Mwaikugile aliithibitishia Mahakama kuwa aliitoa shilingi laki moja kama fedha ya mafuta ya pikipiki kwaajili ya kumtoa Bw.Kongo kutoka Luilo hadi Ludewa Mjini ili kusafisha njia ya kupata zabuni.

Mh.Hakimu alisema kutokana na ushahidi wa mtoaji fedha haioneshi kama Bw.Kongo aliiomba fedha hiyo zaidi ya Bw.Mwaikugile kumshawishi ili aweze kuunganisha na wajumbe wa bodi ya zabuni ili afanikiwe mambo yake.

Mh.Lukuna alisema kwa upande wa mwenyekiti wa wilaya ya Ludewa wa bodi ya zabuni Bw.Lazaro Mapunda alikiri mbele ya mahakama kuwa Bw.Kongo hakuwa mjumbe wa bodi hiyo hivyo alikuwa hana uwezo wa kumpatia uzabuni mkandarasi.

Alisema kesi hiyo imesikilizwa upande wa mashtaka pekee na jumla ya mashahidi nane walitoa ushahidiambapo kupitia sheria katika kifungu 15 A na B ya kuomba na kupokea rushwa ya kuzuia na kupambana na rushwa sheria namba 11 ya mwaka 2007 ndiyo iliyoamuru Bw.Kongo kuachiwa huru.

“kutokana na vielelezo zilivyotoleawa pamoja na ushahidi uliotolewa na upande wa mashtaka na kushindwa kuthibitisha kama Bw.Kongo anakesi ya kujibu na kupitia vifungu vya sheria ya kuomba na kupokea rushwa mahakama inamuachia huru kwakua hana kesi ya kujibu”,alisema Mh.Lukuna.

Awali ilidaiwa mahakamani hapo kuwa kati ya oktoba mwaka jana na machi mwaka huu mshtakiwa Matei Kongo aliomba rushwa kwa  Samson Mwaipugile mkazi wa Dar es Salaam ili aweze kumpa kwa upendeleo tenda ya ujenzi wa barabara na kusambaza vifaa vya ofisi ikiwemo komputa katika halmashauri ya wilaya ya Ludewa.

Mwenyekiti huyo wa halmashauri ya wilaya ya Ludewa alikamatwa na kufikishwa mahakamani kwa madai kuwa machi 12 mwaka huu alipokea rushwa ya shilingi laki moja (100,000) kwanjia ya benki ya NMB Tawi  la Ludewa kupitia akaunti ya Aidan Luoga.

Katika hali iliyowashangaza wasikilizaji shahidi wa mwisho katika kesi hiyo ambaye anatajwa kuwa rafiki mkubwa wa mshtakiwa Bw Aidani Luoga akaiambia mahakama kuwa machi 12 mwaka huu mshtakiwa alikwenda kwake kuomba namba ya akaunti ya NMB akampa lakini akashangaa siku hiyo majira ya saa 9 mchana akakamatwa na takukuru.

Kwa upande wa mashtaka yaani taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa(TAKUKURU)kesi hiyo ilisimamiwa na mwanasheria msomi Bi. Restuta Kessy  na kwa upande wa mshtakiwa ilisimamiwa na wakili wa kujitegemea Bw. Frank Ngafumika mpaka ilipofikia tamati. 

Mwisho.

No comments: