Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

March 04, 2013

SHIRIKA LA MISO KUPITIA WAFADHIRI WAKE LAMSAIDIA MTOTO JULIANA MWINUKA




                   
 Mtoto Juliana Mwinuka baada ya kuwekewa ngozi nyingine usoni,kulia ni mfadhiri wake Bi.Mariam Masawe kushoto ni bibi yake Magreti Mahanje.
Mtoto Juliana akiwa katika hali ya kuridhisha baada ya matibabu
Huyu ndio Bi.Jemidah Kulanga aliye mtafutia mfadhiri mtoto Juliana hapo akiwa na mtoto huyo katika Hospitari ya Taifa ya Muhimbili
Kushoto ni Bw.Katambala akisaidiana na bibi wa mtoto Juliana wakimnywesha uji hospitari ya CCBRT


Katikati Mtoto Juliana Mwinuka kulia ni Bw.Katambala na kushoto ni Bi.Magreth Mahanje wakiwa katika gari ya mfadhiri Bi.Mariam wakielekea katika Hospitari ya Taifa ya Muhimbili.
Kushoto Bi.Jemida Kulangaakuhudhuria kikao ndipo alipo pata picha ya Mtoto Juliana Mwinuka na kumuunganisha kwa Mfadhiri.
Mtoto Juliana baada ya Matibabu
Mtoto Juliana Mwinuka kabla ya matibabu
          Tunaomba radhi kwa picha hizi.

 Shirika lisilo la Kiserikali la MISO(Milo Sayuni Ophans) Lenye makao yake makuu wilayani Ludewa katika mkoa wa Njombe linatoa shukrani za dhati kwa wadau mbalimbali walioshiriki kwa namna moja au nyingine katika michango yao iliyomwezesha mtoto Juliana Mwinuka aliyeungua moto kwaajili ya matibabu.

Akiongea na waandishi wa habari leo Afisa tathmini na ufuatiliaji wa shirika la MISO Bw.Geofrey Katambala alisema shirika hilo kupitia mradi wa Africare waliweza kumuibua mtoto huyo katika kijiji cha Mbugani kata ya Mavanga wilayani Ludewa na kutafuta wadhiri walioweza kumsaidia.

Alisema haikuwa kazi rahisi kumpata mfadhiri lakini kutokana na nguvu za Bi.Jemida Kulanga aliweza kuliunganisha shirika hilo na wakinadada wawili ambao ni Bi.Mariam Masawe na Halima Mohammed lakini safari ya ufadhiri wa Juliana pale ambapo mmjoa wa wafadhiri hao Bi.Halima Mohammed kufariki dunia kwa ajari ya gari.

Bw.Katambala alisema alibaki mfadhiri mmoja ambaye ni Bi.Mariam ambaye aliendelea kutoa msaada kuanzia mtoto huyo alipo fikishwa katika hospitari ya Taifa ya Muhimbili na baadae kuhamishiwa katika hospitari ya CCBRT kwaajili ya kuwekewa ngozi nyingine usoni kutokana na uso wa mtoto huyo kuteketea kwa moto.

“Tunawashukuru wadau mbalimbali kutokana na misaada yao ya hali na mali hasa Bi.Mariam Masawe,Bi.Jemida Kulanga na mwanahabari Francis Godwin kupitia mtandao wake kwani wadau waliweza kuziona picha za mtoto huyo na kuguswa na jambo hilo”,alisema Bw.Katambala.

Alisema mpaka sasa mtoto huyo ameweza kutibiwa vizuri na kurudishiwa ngozi ya uso wake na yupo kijijini kwake na anaendelea vizuri akihudumiwa na bibi yake Magreth Mahanje wakiendelea na kilimo cha zao la mahindi.

Aidha Bw.Katambala aliwataka wadau kuendelea kumchangia mtoto huyo kwa bado anahitajika kurudi hospitari baada ya miezi mitatu ili kuendelea kufanyiwa upasuaji na ubandikaji wa ngozi maeneo mengine hasa maeneo ya jicho lake la kulia.

Alisema jicho la kushoto liko sawa lakini jicho la kulia bado lina matatizo hivyo madaktari walishauri kuwa ataendelaa kupata matibabu ili aweze kurudi katika hali yake kwani bado ana umri mdogo anaweza kufanya shughuri za uzalishaji baadae.

Hata hivyo shirika la miso linampango wa kumuanzisha shule ili apate elimu itakayo weza kumsaidia katika maisha yake kwani anauwezo mzuri akipata msaada wa kuendelezwa kielimu.

Mwisho.

No comments: