Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

October 02, 2012

UKOSEFU WA PETROL NJOMBE WAWA KERO KWA WAMILIKI WA VYOMBO VYA MOTO

Na Nickson Mahundi ,Njombe.

Kwa siku ya tatu sasa mji wa njombe umekumbwa na adha ya kukosekana kwa nishati ya mafuta ya petrol kwenye vituo vya mafuta hali inayopelekea kukwama kwa usafiri na kushuka kwa uchumi miongoni mwa jamii.

Hali hiyo ilitokea septemba 30 mwezi uliopita hadi sasa ambapo hadi hii leo ni kituo kimoja cha ndime petrolstation pekee ndicho kilichofanikiwa kuleta aina hiyo ya mafuta.

Wakizungumza na mwandishi wetu jana kwa nyakati tofauti baadhi ya madereva wa magari na pikipiki mjini njombe wamesema kuwa adha hiyo imepelekea baadhi ya magari na pikipiki kuzima njiani yakiwa na abiria kitu ambacho kimeleta usumbufu kwa abiria.

 Meneja wa kituo cha  ndime petrolstation,Bw.Prosper Mtewele na kaimu meneja wa kituo cha mafuta total walisema tatizo hilo limetokana na kituo kikubwa cha kusambaza mafuta kutofanya kazi hiyo kwa siku za jumamosi na jumapili.

Kutokana na hali hiyo ndio sababau kubwa ya kukosekana kwa nishati hiyo ambayo imesababisha usumbufu mkubwa kwa wahitaji kwa wamekuwa wakitumia muda mrefu katika foreni ya kupata nishati hiyo.

“kutokana na wasambazaji wakuu kutofanya kazi siku za jumamosi na jumapili imepelekea tatizo hili lakini wanashindwa kutambua huu sasa ni mkoa na si kama ilivyokuwa awali,tunapata usumbufu mkubwa kwa wateja”,alisema meneja Mtewele.

Hat hivyo pamoja na kutokuwepo kwa mafuta mjini njombe hakuna ongezeko lolote la bei ya mafuta lililo ongezeka mkoani hapa.

Aidha madereva wamekerwa na kulazimika kununua mafuta katika wilaya na mikoa ya jirani wawapo safarini ili kuepuka usumbufu wanaoupata Njombe.

MWISHO

No comments: