Na Nickson Mahundi,Njombe.
Serikali ya
Tanzania kupitia shirika la umeme tanesco,kwa kushirikiana na mwekezaji kutoka
nchini marekani, inajiandaa kutekeleza mradi wa umeme wa maji katika mto
ruhuji.
Akizungmza
jana kwenye baraza la madiwani, mpimaji
ardhi mwandamizi wa shirika la tanesco
makao makuu Hamis Boby alisema mradi huo unatarajiwa kukamilika hadi kufikia
mwaka 2019 na kuzalisha umeme wa megawati takribani mia tatu hadi mia nne.
Bw.Boby
alisema mradi huo utahusisha ujenzi wa mgodi wa kufua umeme wa megawati 350
hadi 500,bwawa la kuhifadhi maji ,bwawa la kuzalisha umeme,njia ya
umeme,barabara,njia ya kusafirisha maji chini ya ardhi,ofis na makazi.
Hata hivyo
alisema hatua hiyo itazingatia haki za wananchi katika eneo husika kwa kulipwa
fidia ya ardhi,kupata huduma za kijamii,elimu ya mahusiano,pamoja na huduma
nyingine zitakazopendekezwa kwenye makubaliano yao na wadau.
Akizungumzia
malalamiko kuhusu fidia kwa wananchi, mpimaji huyo wa ardhi mwandamizi wa shirika la tanesco makao makuu
alisema utaratibu wa kutoa malalmiko hayo utapitia kwenye uongozi wa vijiji
kabla ya kupelekwa kwa mkurugenzi wa wilaya afisa ardhi na tanesco ambapo
tanesco na wataalam wa halmashauri watashughulikia malalamiko hayo.
Kwa upande
wao madiwani wa halmashauri ya Mji Njombe na wilaya Njombe waliupongeza mpango
huo wa serikali na kuwataka wawekezaji hao kutoa fidia kwa wananvhi wa maeneo
husika bila kujali dini kabila wala rangi.
Akifunga
kikao hicho mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Njombe Venancy Kabelege
aliwataka madiwani kushirikiana na serikali katika kuwahamasisha wananchi ili
kufanikisha zoezi hilola mradi.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment