Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

September 30, 2012

UCHAGUZI CCM WILAYA YA LUDEWA WAMALIZIKA KWA TAABU


Na Nickson Mahundi,Ludewa


Mvutano wa wanasiasa ndani ya Chama Cha Mapinduzi umezidi kushika kasi katika chaguzi mbalimbali za chama hicho nchini mbapo jana katika wilaya ya Ludewa mvutano huo uliendelea katika nafasi ya Halmashauri kuu ya CCM(NEC).
 
Katika mvutano huo wilaya Ludewa wagombea walionekana kugongana katika matokeo ya uchaguzi kwa ngazi ya NEC ndipo wajumbe walipotakiwa kurudia kwa mara ya pili ili kufanikisha kumpata mwakilishi kutoka wilayani humo

Wagombea wa NEC walikuwa watatu ambao ni Bi.Elizabeth Haule,Bi.Angera Libato na Mhandisi.Zefania Chaula lakini mvutano mkali ulikuwa kwa wagombea wawili ambao ni Elizabeth Haule na Zefania Chaula kwa kugongana matokeo yao ya kura za awali

Lilipo rudiwa zoezi la upigaji kura ndipo Bi.Elizabeth Haule aliibuka mshindi kwa kura 592 na kuwa mwakilishi wa NEC huku mhandisi Zefania Chaula akipata kura 452 akishindwa kuamini kuhusiana na matokeo hayo na kutokukubaliana nayo.

Mhandishi Chaula alilalamikia kutotendewa haki katika uchaguzi huo na kusisitiza mbele ya wajumbe kuwa atafuata ngazi husika na kuyapeleka malalamiko yake ili kutambua ukweli wa matokeo hayo kwa kanuni ya katiba ya CCM.

Aidha msimamizi Mkuu wa uchaguzi huo Bw.Valensia Kabelege aliwaambia waandishi wa habari kuwa uchaguzi huo ulikuwa wa huru na haki kama ilivyotakiwa katika kanuni za chama cha mapinduzi na kumtaka mhandisi Chaula kufuata ngazi za kisheria kama hakuridhika na matokeo hayo.

“uchaguzi umekwenda vizuri kama ilivyotakiwa ufanyike na kama kuna mtu yeyote hajaridhika na matokeo haya basi anaweza kufuata ngazi husika ili kutoa vielelezo vitakavyoonesha mapungufu yaliyojitokeza”,alisema Bw.Kabelege.

Wengine walioshinda katika ngazi mbalimbali ni Felix Haule katibu siasa na uenezi,Halmashauri kuu ya wilaya kupitia wazazi ni Donald Mwalongo,Hilary Nkwera,Mathei Mtweve na Stanley Gowele.

Mbunge wa zamani wa jimbo la Ludewa na Mkuu wa wilya ya Tarime mstaafu Bw.Stanley Kolimba alichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Ludewa,wajumbe mkutano mkuu wa taifa ni,Monika Mchilo,Stanley Gowele,Leodiga Mpambalyoto,Elisha Haule na Adalubeti Mgimba.

Waliochaguliwa mkutano mkuu wa Mkoa ni Selina Haule,Donald Mwalongo na Oigeni Lugome aidha uchaguzi huo ulimalizika majira ya saa sita usiku ndipo matokeo hayo yalipotangazwa na wajumbe kurejea vijijini kwao.

MWISHO.

No comments: