Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

October 10, 2012

ROSE LWIVA AIBUKA KIDEDEA KATIKA UCHAGUZI UWT MKOA WA NJOMBE

 Umoja wa jumuiya ya Wanawake wa cha cha mapinduzi Tanzania UWT kwa mkoa wa Njombe jana umefanya uchaguzi wa viongozi katika ngazi mbalimbali za viongozi wa mkoa ambapo katika uchaguzi huo Rose Mery Lameck Lwiva aliweza kumubwaga scolastika christian Kevela kwa kupata kura 190 kwa 164 kati ya wapiga kura 354.


Miongozi mwa nafasi za uongozi zilizowaniwa na wagombea wa umoja huo wa wanawake ni pamoja na nafasi ya mwakilishi UWT kwenda umoja vijana ccm mkoa wa Njombe,mkutano mkuu wa ccm mkoa,mkutano mkuu wa taifa,umoja wa wanawake kwenda wazazi mkoa na baraza la mkoa.

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa na Njombe Deo Sanga ambaye ni mbunge wa Jimbo la Njombe Kaskazini amesema matokeo hayo yasilete mgawanyiko katika chama ili kuepusha upinzani kushika dola mwaka 2015.

Rose mary ashukuru usimamizi ulivyofanyika vizuri hadi kupelekea ushindi mnono kwake haku akieleza jitihada zilizofanywa na mwenyekiti anayemaliza muda sasa kwa kipindi chote.

Awataka Madiwani kushikamana kuujenga mkoa wa Njombe huku akiahidi kuwa sambamba na akinamama katika kujenga chama.

Katibu wa ccm mkoa wa Njombe bwana Hosea Mpagike asema Rufaa iko wazi kwa muda wa siku 14 Kama yupo mwenyemalalamiko

Mama scolastika kevela asema kura 164 alizozipata ni kuwaheshimu akinamama wa UWT huku akimtupia lawama mshindi kuwa siku moja kabla ya uchaguzi aligawa vitenge wilaya ya Makete pamoja na kufanya mambo mengi kikiwemo chakula.


No comments: