Social Icons

Facebook Twitter LinkedIn Google+

October 10, 2012

CHAMA CHA WAANDISHI WA HABARI MKOA WA NJOMBE(NPC) CHAPATA UONGOZI

Chama cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Njombe, Njombe Press Club NPC Leo Kimefanya Uchaguzi wa Viongozi wa Muda wa Chama Hicho Ambapo Bazil Makungu Amechaguliwa  Kuwa Mwenyekiti wa NPCkwa kushinda kwa kura 20 19 kati ya 20 zilizopigwa Huku Ellymathew Kika Akichaguliwa Kuwa Makamu Mwenyekiti kwa kushinda kura 8 na kuwabwaga wagombea wenzake watatu..

Akitangaza Matokeo ya Uchaguzi Huo Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi Huo Shaban Lupimo Amesema Mwenyekiti wa Muda wa NPC Bazil Makungu Amepata Kura 19 Kati ya Kura 20 Zilizopigwa  Huku Kura Moja Ikiharibika.

Amesema kwa nafasi ya katibu wa chama hicho Ndg.Hamis Hassan Kassapa ameshinda kwa kura 15 kati ya 18 zilizopigwa na tatu kuharibika kutokana na mgombea kuto kuwa na mpinzani huku Lilian Mkusa akichaguliwa kuwa makamu Katibu.

Katika nafasi ya uhasibu Sunday Bavuga amechaguliwa mara baada ya kukosekana kwa mpinzani huku Consolatha kihombo akichaguliwa kuwa makamu wake.

Kwa Upande Wake Msimamizi Mkuu wa Uchaguzi Huo Fedrick Siwale ametangaza Majina ya Wajumbe wa Kamati Kuu Tendaji wa Njombe Press Club watakao ingia kwenye kamati hiyo.

Wajumbe hao ni wale saba watakaokamilisha safu ya watendaji 13 wa chama hicho ambao ni pamoja na Festus Pangan,Nickson Mahundi,Gabriel Kilamlya,Riziki Manufred,Amos Kaposo,Martha sanga pamoja na Mercy James,

Awali Akizungumza Kabla ya Uchaguzi Huo  Mgeni Rasmi Deo Haule Filikunjombe Ambae ni Mbunge wa Jimbo la Ludewa Amewataka Waandishi wa Habari Kufanyakazi Kwa Zingatia Maadili, Mipaka, Misingi ya Taaluma Yao Pamoja na Kutumia Weledi Walionao.

Katika Hatua Nyingi Filikunjombe Ameahidi Kutoa Vifaa Kwa Ajili ya Ofisi ya Waandishi wa Habari Zikiwemo Kompyuta Ndogo (Laptop), Printer na Scannaer pamoja na vifaa vingine.

Akizungumza Kwaniaba ya Viongozi Waliochaguliwa Mwenyekiti wa NPC  Bazil Makungu Amewashukuru Wajumbe wa Chama Hicho na Kuwataka Kuwa na Ushirikiano Kati Yao na Viongozi Waliowachagua Ili Kufanikisha Malengo  ya Chama Hicho.

Uchaguzi Huo Umehudhuriwa na Wageni Kutoka Chama cha Waandishi wa Habari wa Mkoa wa Iringa ICP Akiwemo Katibu wa  ICP Frank Leonald
..........................................................................................................................

No comments: